• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Maji

IDARA YA MAJI.

Idara ya Maji ni moja kati ya Idara zilizoko Katika Halmashauri ya Sengerema zenye majukumu yafuatayo:-

  • Kusanifu na kusimamia ujenzi na ukarabati wa Miradi ya Maji.
  • Kuunda vyombo vya watumiaji maji ili wananchi waweze kusimamia na kuendesha miradi yao ya maji katika ngazi ya jamii.
  • Kushirikiana na wadau mbalimbali ili kupata fedha na kutekeleza miradi mikubwa ya jamii ya kuwahudumia jamii.
  • Kutoa elimu kwa umma kwa njia mbalimbali juu ya hifadhi ya mazingira na uendeshaji wa huduma ya maji.
  • Kushirikiana na Mamlaka ya Maji Sengerema, katika utekelezaji wa Mpango wa muda mrefu kuboresha vyanzo vya maji vilivyopo ikiwa ni pamoja na uanzishwaji wa vyanzo vipya vya maji.

Malengo/Majukumu ya Idara ya Maji

Kuandaa bajeti ya kutekeleza miradi ya maji na kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo

Kutoa huduma ya maji safi na salama kwa wakazi wa Halmashauri wasiopata huduma ya maji kutoka kwa mamlaka ya Maji Sengerema.

Kutoa mafunzo, kusimamia mchakato wa kuunda vyombo vya kusimamia na kuendesha miradi ya maji pamoja na kuvisajili, kwa mujibu na taratibu wa Sheria ya Maji ya 2009.

Kuendesha miradi ya maji kutunza fedha za matengezo na kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha za mfuko.

Kupunguza na kuzuia milipuko ya magonjwa yanayosababishwa na ukosefu wa maji safi na salama

Kusimamia vyema miradi inayofanya kazi kwa kusisitiza vyombo vya kusimamia

Idara inahusika na kupanga na kusanifu miradi ya maji, kupitia usanifu wa miradi ya maji unaofanywa na wataalam wa nje, kusimamia ujenzi na uendeshaji wa miradi ya maji pamoja na kukarabati miradi ya maji yenye hitilafu. Idara pia inahusika na kuunda na kusimamia vyombo vya watumiaji maji

BODI ZA WATUMIA MAJI.

Idara ya maji imeendelea kukabiliana na changamoto ya miradi mingi ya maji iliyoko vijijini kutofanya kazi vizuri kutokana na sababu mbalimbali, zikiwemo kutosimamiwa vizuri na kukosa matengenezo muhimu. Kutokana na dhana kuwa jukumu la kuwapatia wananchi huduma ya maji ni la Serikali pekee, Upungufu huo umesababisha kuhitajika kwa mpango thabiti na endelevu wa uratibu na usimamizi wa utoaji wa huduma hii katika ngazi ya halmashauri ya kuunda Bodi za watumia maji na kuzipa mafunzo pamoja na kusajili Bodi hizo.

MSAJILI WA BODI ZA WATUMIA MAJI HALMASHAURI YA WILAYA

kupitia Sheria ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira Na.12 ya mwaka 2009. Halmashauri za Wilaya, ina mamlaka ya kuteua msajili na kusimamia mchakato mzima wa usajili chini ya Sheria ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira, iliyoanza kutumika rasmi tarehe 1.8.2009.

Katika Halmashauri ya Bagamoyo Msajili wa bodi hizi ni Mwanasheria wa Halmashauri ya Bagamoyo.

UUNDAJI NA USAJILI WA VYOMBO VYA WATUMIAJI MAJI

(i) Kamati ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Kijiji au Kamati ya Maji kwa kushirikiana na Wataalam Washauri au Timu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Wilaya itaitisha kikao cha awali ili kuweka bayana na kujadili wazo la kuunda chombo cha watumiaji maji kwa miradi iliyokwishakamilika, inayoendelea kujengwa au itakayojengwa.

(ii) Kamati ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Kijiji itaafikiana kuhusu kuunda chombo cha watumiaji maji na uamuzi huo utawasilishwa kwenye mkutano mkuu wa kijiji.

(iii) Washauri au Timu ya Wataalam wa Maji na Usafi wa Mazingira ya Wilaya wataelimisha wananchi katika vikao mbalimbali vitakavyoandaliwa, kuhusu umuhimu wa kuunda vyombo vya watumiaji maji vilivyosajiliwa kisheria, aina mbalimbali za vyombo vya watumiaji maji, kuwaongoza na kutoa ushauri katika mchakato wa kuchagua aina ya chombo wanachokipenda, taratibu na hatua za usajili kwa kila aina ya chombo. Chombo cha watumiaji maji kitaanzishwa baada ya wananchi kukubaliana kwa pamoja kwa kuzingatia masharti au vigezo vinavyotawala katika aina ya chombo kitakachochaguliwa.

(iv) Mkutano wa wanakijiji wote utaitishwa ili kuamua kwa pamoja, kwa mujibu wa walio wengi, kuunda aina ya chombo cha watumiaji maji wanachoona kinawafaa kwa mujibu wa maelekezo ya wataalam wa wilaya. Mkutano huo utateua kamati ya muda itakayokuwa na viongozi waanzilishi kwa kuzingatia usawa wa kijinsia watakaosimamia uundaji wa chombo cha watumiaji maji.

Endapo chombo cha watumiaji maji kitahusisha zaidi ya kijiji kimoja, maamuzi ya wananchi katika kila kijiji yatajadiliwa katika kamati ya muungano yenye wawakilishi wa wananchi kutoka kila kijiji.

(v) Viongozi waanzilishi watasimamia shughuli ya kuandaa rasimu ya katiba na kanuni za chombo kilichopendekezwa.(rejea katiba ya mfano ambayo imeambatanishwa kwenye mwongozo huu). Kwa mujibu wa mwongozo huu, uandaaji wa rasimu ya katiba na kanuni utamshirikisha Mhandisi wa Maji, Afisa Maendeleo ya Jamii na Mwanasheria wa Halmashauri husika.

(vi) Viongozi waanzilishi walioteuliwa watawasilisha rasimu ya katiba na kanuni kwenye mkutano mkuu wa wanakijiji wote ili kujadiliwa na kupitishwa na mkutano huo.

Iwapo chombo kinachotarajiwa kuundwa kitahusisha kijiji zaidi ya kimoja, rasimu na katiba ya chombo itawasilishwa katika mkutano wa pamoja utakaowajumuisha wawakilishi wa wananchi kutoka vijiji husika, ambao kwa pamoja watafikia maamuzi.

(vii) Pia, viongozi waanzilishi watawasilisha nakala ya rasimu ya katiba na kanuni kwenye kikao cha maendeleo ya kata kwa taarifa, kumbukumbu na pia ili kuthibitisha kutokuwepo kwa pingamizi ndani ya kata. Hii itawezesha kubaini kuwepo au kutokuwepo kwa jumuiya kama ile inayopendekezwa ndani ya kata.

(viii) Baada ya kupitishwa kwa rasimu za katiba na kanuni, mwenyekiti na katibu wa kamati ya muda watawasilisha kwa Mkurugenzi wa Halmashauri rasimu ya katiba, kanuni na nyaraka zote zinazotakiwa kwa ajili ya uundaji wa chombo cha watumiaji maji, ili kipate ridhaa ya Halmashauri. Mkurugenzi wa Halmashauri ana uhuru wa kufanya ukaguzi au uchunguzi wowote anaouhitaji kupitia wataalam wake ili kujua hali halisi, kabla ya kuwasilisha ombi la kuunda chombo kwenye kamati au vikao husika kwa ajili ya kupata ridhaa.

(x) Mkurugenzi wa Halmashauri atakiandikia barua chombo husika kilichoundwa, akionyesha kuwa Halmashauri imetoa ridhaa ya kuundwa kwa chombo husika katika kijiji/vijiji kilichowasilisha maombi hayo, akiambatanisha majina ya viongozi waanzilishi (Mwenyekiti, Katibu na Mweka Hazina) wa chombo husika kwa kuzingatia matakwa ya katiba na atatoa nakala kwa Afisa Mtendaji wa Kata na Afisa Mtendaji wa Kijiji.

(xi) Kufikia hatua hii, chombo cha watumiaji maji tayari kitakuwa kimeundwa kulingana na katiba na kanuni walizojiwekea, tayari kwa hatua za usajili.

USAJILI WA VYOMBO VYA WATUMIAJI MAJI

(i) Viongozi wa chombo cha watumiaji maji watawasilisha fomu ya maombi ya kusajili chombo cha watumiaji maji kwa Msajili na kutoa nakala kwa Afisa Mtendaji wa Kijiji na Afisa Mtendaji wa Kata, wakiambatanisha katiba na kanuni ya chombo hicho na muhtasari wa mkutano mkuu wa wanakijiji/wanavijiji wote pamoja na majina ya wajumbe waliohudhuria na sahihi zao na nakala ya barua kutoka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri inayoonyesha kuwa Halmashauri imeridhia uundaji wa chombo hicho.

(ii) Waombaji watalipia ada ya usajili wa chombo cha watumiaji maji kama itakavyopangwa na Msajili wa Vyombo vya Watumiaji Maji wa Halmashauri.

(iii) Msajili atahakiki uhalali wa chombo cha watumiaji maji kilichofuzu vigezo vilivyotakiwa kwenye usajili na kutoa mapendekezo au ushauri kwa chombo ambacho hakikufuzu ili kizingatie vigezo na kiweze kufuzu.

(iv) Wananchi watafahamishwa kuhusu matokeo ya uhakiki iwapo maombi yao yanafuzu vigezo vilivyowekwa au kama yanahitaji maboresho kabla ya kusajiliwa.

(v) Msajili atatoa hati ya kisheria ya usajili kwa chombo cha watumiaji maji kilichofuzu vigezo vilivyotakiwa ili kitambulike kisheria na kuweza kutekeleza majukumu yaliyokusudiwa kwa mujibu wa sheria.

(viii) Msajili atatoa taarifa kwa Mkurugenzi wa Halmashauri kuhusu maombi yaliyopokelewa, kuhakikiwa, kukubaliwa na kusajiliwa ama kukataliwa.

(ix) Waombaji ambao maombi yao yamekataliwa wanayo haki ya kukata rufaa kwa Mkurugenzi wa Halmashauri baada ya kulipa ada kama itakavyopangwa na msajili.

Baadhi ya Maeneo yaliyopo ndani ya Halamsahauri ambayo yana miradi ya maji inayoendelea

Mradi wa maji buyagu, kalangalala, Bitoto

Bonyeza Hapa.pdf

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.