• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI MKUU ASIFU MAENDELEO YA SENGEREMA

Posted on: May 19th, 2025


Ataka Halmashauri kuanzisha miradi ya kimkakati


Aweka Jiwe la Msingi Hospitali ya Halmashauri, Jengo la Utawala


Daraja la JP Magufuli kuzinduliwa na Dkt. Samia Juni 19, 2025



*Umoja wa Bodaboda Sengerema Wachangiwa Milioni 50 Kununua Gari la Abiria


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amesifu jitihada za Serikali wilayani Sengerema kwa kusimamia vyema fedha za miradi ya maendeleo ambapo amesema Wilaya ya Sengerema imepiga hatua kubwa kimaendeleo ndani ya muda mfupi ambapo ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kuanzisha miradi ya kimkakati ili kuvutia wadau mbalimbalimbali wa maendeleo wakiwemo watalii.


Pongezi hizo zimetolewa na Waziri Mkuu  Mei 19, 2025 wakati wa ziara yake wilayani Sengerema kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya stendi ya zamani mjini Sengerema.


Waziri Mkuu amesema kutokana na kasi ya maendeleo iliyopo Sengerema pamoja kukamilika kwa daraja la Kigongo Busisi kukamilika  na Mgodi mkubwa uliopo Nyanzaga, viongozi wa Halmashauri wanatakiwa kuwa wabunifu kwa kuanzisha miradi ya kimkakati likiwemo soko la kisasa, stendi pamoja na maegesho ya magari ili kuvutia wafanyabiashara mbalimbali pamoja na watalii kuja wilayani Sengerema kuwekeza.


"Niwapongeze kwa ujenzi wa Soko na stendi, Sengerema inakua kwa kasi, ninyi hamuwezi kuona,  Sengerema imakuwa kwa kasi, Sengerema ni mji wa kibiashara, Sengerema kuna idadi kubwa ya watu, na kuna mgodi mkubwa utaanza hivi karibuni, hapa patakuwa hapashikiki" amesema Waziri Mkuu


Wakati huo huo Waziri Mkuu amepongeza jitihada za umoja wa Bodaboda Wilayani Sengerema kwa kuamua kununua gari la abiria ambapo yeye mwenye, viongozi  na umoja wa Bodaboda wamechangia kiasi cha shilingi milioni 50 kuwezesha upatikanaji wa gari hilo.


Waziri wa Ujenzi Mhe. Abdallah Ulega amesema ujenzi wa daraja la Kigongo Busisi lenye urefu wa kilometa 3 kwa sasa umekamilika, ambapo amesema sasa litazinduliwa rasmi tarehe 19 Juni, 2025 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan hivyo amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi siku hiyo.


Mbunge wa jimbo la Sengerema Mhe. Hamis Tabasam amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwezesha utekelezaji wa miradi mingi ya maendeleo katika jimbo la Sengerema ambapo amemwomba Waziri Mkuu kusaidia upatikanaji wa fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa hospitali ya Wilaya iliyopo Mwabaluhi kwa kujenga uzio pamoja na nyumba za watumishi.


Mapema Waziri Mkuu aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali ya Hamashauri pamoja na jengo la utawala lililopo Bomani.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • WAZIRI MKUU ASIFU MAENDELEO YA SENGEREMA

    May 19, 2025
  • DED SENGEREMA AGUSWA NA KERO ZA WATUMISHI

    May 02, 2025
  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.