• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

WATENDAJI SENGEREMA WATAKIWA KUTOA KIPAUMBELE ELIMU YA LISHE

Posted on: November 8th, 2024


*Mashamba ya Shule Yatumike kwa ajili ya Chakula cha Wanafunzi


Watendaji wa kata za Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema wametakiwa kutoa  kipaumbele elimu ya lishe katika jamii hususan suala la wazazi kuchangia chakula katika shule wanazosoma watoto wao ili kufanikisha suala la kuboresha  hali ya lishe na kupunguza athari za utapiamlo katika jamii.


Agizo hilo limetolewa leo na Katibu Tawala Wilaya ya Sengerema, Curthbert Midala kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya kwenye kikao cha kamati ya lishe kwa ajili ya kujadili taarifa za kipindi cha Mwezi Julai hadi Septemba 2024 kilichofayika kwenye ukumbi wa Sengerema Sekondari.


Katibu Tawala amesema elimu ya Lishe katika jamii inapaswa kupewa kipaumbele ili jamii iweze kubadilika na kuwa na mtizamo chanya kwenye suala zima la lishe.


"Suala la lishe linapaswa kuzingatiwa na kuwa agenda zenu za kila siku, hata sisi kwenye vikao vyetu, lishe ni agenda ya kudumu" amesisitiza Katibu Tawala.


Kwa upande mwingine Katibu Tawala amewataka watendaji kuendelea kuhamasisha wazazi na walezi wa wanafunzi kuendelea kuchangia chakula kwenye shule wanazosoma watoto wao pamoja na kuhakikisha wanasimamia maadhimisho ya siku ya lishe katika vijiji ili jamii iweze kupata uelewa wa masuala ya lishe ambapo itasaidia kubadili tabia na mitizamo juu ya lishe.


Katika kuhakikisha wanafunzi wanapata chakula shuleni, Katibu Tawala ameagiza mashamba yote yanayomilikiwa na shule yatumike kwa ajili ya manufaa ya wanafunzi ambapo pia ameshauri kutoa motisha kwa kata zinazofanya vizuri kwenye viashiria na malengo ya lishe.


Mapema akitoa maelezo mafupi ya kikao hicho, Mganga Mkuu wa Halmashauri, Fredrick Mugarula amesema Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema inafanya vizuri kwenye malengo 13 ya Lishe ambapo amesema eneo ambalo limekuwa na changamoto ni utoaji wa chakula shuleni pamoja na upatikanaji wa fedha kwa ajili ya shughuli mbalimbali za lishe.


Wakichangia katika kikao hicho, Watendaji  wa kata wamesema wazazi na walezi wamekuwa wagumu kuchangia vyakula shuleni kutokana na sababu mbalimbali, hivyo wameomba uongozi wa Wilaya uweze kutoa tamko ili jamii ilazimike katika uchangiaji wa vyakula shuleni.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.