• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

WATENDAJI KATA SENGEREMA WANUFAIKA NA PIKIPIKI

Posted on: February 27th, 2023

Jumla ya watendaji 8 wa kata za Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema wamenufaika na pikipiki zilitolewa na

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa lengo kuboresha mazingira ya utendaji kazi kwa maofisa hao.


Akikabidhi pikipiki hizo, Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Senyi Ngaga amewataka watendaji hao kutumia vizuri Pikipiki hizo ili ziweze kufikia malengo yalikusudiwa na Serikali ikiwemo ukusanyaji wa mapato pamoja utoaji wa huduma mbalimbali kwa wananchi.


"Pikipiki hizi zimenunuliwa kwa kodi za wananchi, ni imani yangu mtazitumia vizuri tena kwa shughuli za Serikali" amesema Mhe. Ngaga.


Katika hatua nyingine Mhe. Ngaga ameliagiza jeshi la Polisi wilayani Sengerema kuhakikisha watendaji hao waliopewa Pikipiki wanapewa mafunzo ya namna bora ya utumiaji wa Pikipiki hizo na amewaagiza watendaji hao kuhakikisha wanakuwa na leseni za kutumia vyombo hivyo.

Mhe. Ngaga ameishukuru Serikali kwa kuwajali watumishi ambapo amesema ndani ya mwaka mmoja Serikali imetoa Pikipiki 83 kwa watumishi wakiwemo maafisa kilimo na watendaji wa kata za Halmashauri ya Sengerema na Buchosa


Mapema akimkaribisha Mkuu wa Wilaya kukabidhi Pikipiki hizo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Binuru Shekidele amesema Pikipiki hizo kwa awamu hii ya kwanza zimetolewa kwa watendaji wa kata za pembezoni kwa lengo la kuwasaidia kutimiza majukumu yao ya kila siku ikiwemo ukusanyaji wa mapato.


Mtendaji wa kata ya Chinfunfu Emmanuel Ng'alalile ameishukuru Serikali kwa kuwasaidia usafiri ambapo amesema   umbali kutoka kata hiyo hadi makao makuu ya Halmashauri ni zaidi ya kilomita 50 hivyo itamsaidia katika majukumu yake ya kila siku ikiwemo upelekaji wa taarifa za ofisi pamoja na utoaji wa huduma kwa wakati.


Pikipiki hizo 8 zimekabidhiwa kwa watendaji wa kata za Chinfunfu, Igalula, Kagunga, Buyagu, Kasenyi, Buzilasoga, Igulumuki, na Ngoma.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.