• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

WANAOPISHA MGODI WA NYANZAGA WAANZA KULIPWA FIDIA

Posted on: September 4th, 2023



Zaidi ya Shilingi Bilioni 50 zinatarajiwa kulipwa kwa wananchi 853 wa vijiji vya Sotta na Nyabila vilivyopo kata ya Igalula Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ili kupisha shughuli za uchimbaji Madini ya Dhahabu wa Nyanzanga unaomilikiwa kwa ubia kati Kampuni ya Ore Corp Limited (84%) na Serikali ya Tanzania (16%).


Akizungumza leo Septemba 04, 2023 kwenye hafla ya uzinduzi wa ulipaji wa fidia hizo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi amewaasa  wananchi hao wanaopisha ujenzi wa Mgodi huo kuhakikisha fedha wanazolipwa zinatumika vizuri ikiwemo kujenga makazi bora pamoja na kuanzisha miradi kwa ajili ya kukuza kipato cha kaya.


"Mradi huu ni mkubwa na unatarajiwa kudumu kwa zaidi ya miaka 12, mradi utachangia mambo mengi zikiwemo ajira za moja kwa moja zaidi ya 1000 za wananchi wa maeneo haya na mengine, huu ni uwekezaji mkubwa ambao unakwenda kugusa maisha yenu moja kwa moja" amesema Mhe. Makilagi.


Mhe. Makilagi amesema hatua iliyofikiwa na ulipaji wa fidia kwa wananchi ni ishara nzuri ya kuanza rasmi kwa shughuli za uchimbaji kwenye eneo hilo hivyo ni vyema wananchi hao kuchangamkia fursa kutoka mgodini hapo ambapo pia amewaasa wananchi wa Sengerema kujiandaa na fursa za kiuchumi kama vile ajira na biashara mbalimbali  kutoka mgodini hapo.


Hata hivyo, ametoa wito kwa kampuni hiyo na makampuni mengine yanayofanya kazi na Mgodi kuhakikisha wanalipa  ushuru wa huduma kwa Halmashauri na kodi zote za Serikali kuu kwa wakati.


Msimamizi wa miradi ya kampuni hiyo nchini Isaac Lupokela amesema Mradi wa Nyanzaga utakuwa na manufaa makubwa kwa wakazi wanaozunguka Mgodi, Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema na Taifa kwa ujumla ambapo amesema fedha za kulipa fidia kwa waguswa wote 853 zipo tayari.


Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Sengerema Agustine Makoye amewaasa wananchi ambao bado hawajamilisha ujazaji wa mikataba hiyo kuhakikisha wanakamilisha zoezi hilo ili kutoa nafasi kwa mwekezaji huyo kufanya kazi zake kwa wakati.


Diwani wa kata ya Igalula Mhe. Faustine Shibiliti ameiomba Serikali kutumia busara wakati wa uondoaji wa wananchi hao kupisha mgodi huo ili kuondoa migogoro inayoweza kujitokeza pamoja na uzingatiaji wa ajira za wananchi wanaozunguka mgodi huo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.