• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

WANAFUNZI SENGEREMA KUPATIWA DAWA ZA KINGA YA KICHOCHO NA MINYOO YA TUMBO

Posted on: November 20th, 2023

Zaidi ya wanafunzi 88,000 wenye umri wa kati ya miaka 5-14 wa shule za Msingi 111 za Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema wanatarajiwa kupatiwa dawa za kinga ya dhidi ya magonjwa ya Kichocho na Minyoo ya Tumbo.


Hayo yamebainishwa leo tarehe 20 Novemba, 2023 kwenye kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi kwa ajili ya kujadili uendeshaji wa zoezi la ugawaji wa dawa hizo linalotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 23 na 24 Novemba 2023.


Akifungua kikao hicho Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri Dkt. Fredrick Mugarula kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Sengerema amesema dawa zitakazotolewa kwenye zoezi hilo ni za kawaida na zimekuwa zikitolewa mara kwa mara hivyo amewataka wajumbe wa kikao hicho kwenda kutoa elimu sahihi kwa jamii ili zoezi hilo liweze kuwa la manufaa.


Amesema kutoka na kamati hiyo kuwa na wajumbe kutoka taasisi mbalimbali pamoja na viongozi wa madhehebu ya dini ni vyema ujumbe sahihi ukafika kwa walengwa wakiwemo wazazi wa wanafuzni ili kuweza kuzuia magonjwa ya Kichocho na Minyoo ya Tumbo.


"hizi dawa ni za kawaida, ndiyo hizi hizi hutumika kwenye zahanati zetu, vituo vya afya na hospitali zetu na maduka ya dawa, hivyo hatuna budi kuzitilia mashaka kwani hazina madhara yoyote kwa binadamu" amesisitiza kaimu Mkurugenzi.


Mratibu wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Bibi Rachel Ntogwisangu amesema katika zoezi hilo shule zilizo katika kata 22 zitapata dawa ya kichocho na dawa  ya minyoo ya tumbo na shule katika kata 4 zitapata dawa za minyoo ya tumbo pekee.


Mratibu huyo ameziomba shule zote za msingi kuhakikisha wanandaa chakula kwa wanafunzi wote kabla ya matumizi ya dawa hizo.


Wajumbe mbalimbali waliohudhuria kikao hicho wameuomba uongozi wa Halmashauri kupitia ofisi ya Mganga Mkuu wa Wilaya kuhakikisha walengwa wote wanapatiwa dawa hizo ili kuweza kutokomeza magonjwa yaliyokusudiwa na wamepongeza kwa kikao hicho ambacho wamesema kimesaidia kutoa elimu sahihi kwa wananchi wakiwemo waumini wa madhehebu mbalimbali.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.