• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

WAKWEPAJI CHANJO KUCHUKULIWA HATUA, TAHADHALI YA KIPINDUPINDU YASISITIZWA SENGEREMA

Posted on: February 19th, 2024


Watendaji wa Kata za Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema wametakiwa kuendela kuchukua tahadhali dhidi ya ugonjwa wa Kipindupindu hususan matumizi ya vyoo na mikusanyiko kwenye misiba pamoja na kuwachukulia hatua wazazi wenye watoto ambao hawakupatiwa Chanjo ya Surua na Rubella.

Tahadhali hiyo imetolewa leo (Februari 19, 2024) kwenye kikao kazi kilichowakutanisha watendaji wa kata za Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kwa ajili ya kujadili tathimini ya Kampeni ya kitaifa ya Chanjo ya Surua na Rubella na tahadhali ya Kipindupindu.

Mkurugenzi Mtendaji amewataka Watendaji hao kubadilika na kuacha kufanya kazi kwa mazoea ili kuondoa changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii ikiwemo magonjwa ya mlipuko, ukwepaji wa Chanjo pamoja utoro shuleni.

"Nataka nipate taarifa ya watoto wote ambao hawakupatiwa Chanjo ya Surua na Rubella katika maeneo yenu na mniambie hatua gani mmechukua, watafuteni wote hadi kufikia jioni ya leo nipate taarifa hiyo" amesema Mkurugenzi Mtendaji.

Mkurugenzi Mtendaji amesema suala la kukwepa chanjo ya Surua na Rubella si la kupuuzwa kwani Serikali imetumia gharama kubwa hivyo ni vyema ijulikane sababu ya baadhi watoto katika kata za Katunguru, Kasenyi, Igalula na Nyanchenche kutokupatiwa chanjo hiyo.

Kuhusiana na tahadhali ya Kipindupindu Mkurugenzi Mtendaji amesema mbali na Serikali kupiga marufuku shughuli za matanga na chakula kwenye misiba bado kuna baadhi ya maeneo yanakiuka maagizo hayo kitendo ambacho kitasababisha kuendelea kuwepo maambukizi mapya ya ugonjwa wa Kipindupindu ambao hivi karibuni umeyaathiri baadhi ya maeneo ya Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema.

Watendaji wa kata wamesema mojawapo ya changamoto ya kutofikiwa malengo katika maeneo yaliyotajwa ni pamoja kuhama kwa baadhi ya kaya hususan zile zilizolipwa fidia kupisha shughuli za uchimbaji wa madini katika Kijiji cha Sotta na baadhi ya maeneo yenye wavuvi.

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Dkt. Fredrick Mugarula amesema ugonjwa wa Kipindupindu ni hatari na huambukiza haraka hivyo amewaomba watendaji hao kuendelea kuchukua tahadhali ili kuweza kujikinga na ugonjwa huo ambao kwa muda mfupi tangu mlipuko huo utokee Halmashauri imeweza kutumia gharama kubwa za fedha, nguvu kazi na muda katika kukabiliana na ugonjwa huo hivyo amewataka watendaji hao kuendelea kuchukua tahadhali dhidi ya ugonjwa huo.

 Katika hatua nyingine Dkt. Mugarula amesema katika kampeni ya kitaifa Chanjo ya Surua na Rubella  iliyooanza tarehe 15 hadi 18 Februari, 2024 Halmashauri ilikuwa na lengo la kuwafikia watoto 98,118 lakini imeweza kuwafikia watoto 100,553 sawa na asilimia 102 ya lengo

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.