• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

WAKULIMA KATUNGURU MBIONI KUNUFAIKA NA MRADI WA UMWAGILIAJI

Posted on: September 20th, 2023
  • Zaidi ya wakulima 600 wa kata ya Katunguru Wilayani hapa wanatarajia kuanza kunufaika na mradi wa Umwagiliaji unaotarajiwa kukamilika mwezi Julai 2024 kwa gharama ya shilingi 4,598,267,600.


Hayo yamebainishwa leo tarehe 20 Septemba, 2023 wakati wa kikao cha kujadili mradi huo kilichowakutanisha timu ya wataalamu kutoka Halmashauri, wasimamzi wa mradi na wakandarasi wa mradi huo.


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ndugu Mwita Waryuba amewataka wasimamizi wa mradi huo kuhakikisha wanashirikiana na jamii katika kutoa elimu ya uhamasishaji wa jamii juu ya mradi huo, kuwajibika kwa jamii kwa kurejesha kidogo wanachokipata (CSR) na kutoa taarifa mhimu kwa uongozi wa serikali za vijiji, kata,tarafa na Halmashauri zihusuzo mradi huo.


"Mradi huu umeanza lakini hautakuwa maana kama mtashindwa kushirikiana na jamii inayowazunguka kwa kurudisha sehemu ya mnachokipata kwa kuwezesha baadhi ya miradi kijijini hapa" amesema ndugu Waryuba.


Kwa upande mwingine Kaimu Mkurugenzi huyo amemwagiza msimamizi wa mradi huo kuhakikisha wanarekebisha mapungufu yote yaliyobainika kupitia ziara hiyo pamoja na mkandarasi  kuimarisha ulinzi wa eneo la mradi.


Meneja mradi huo Ombeni Justo Ikola amewaasa wananchi wafugaji wanaozunguka eneo la mradi kutokuingiza mifugo kwenye aneo la mradi ambayo inaweza hatarisha usalama wa mifugo hiyo kutokana na miundombinu iliyopo kwenye mradi huo pamoja na kukwamisha utekelezaji wa mradi huo.


Diwani wa Kata ya Katunguru Mhe. Sadick Jimola amemwomba meneja Mradi wa huo kuhakikisha taarifa za mradi zinawafikia wananchi ili kujua kinachoendelea pamoja na kuzingatia na kuungana na jamii kwenye masuala ya uwajibikaji kwa jamii (CSR).


Mradi wa Umwagiliaji wa Katunguru unaojengwa na kampuni ya SIETCO na JV Jiangxi Geo- Engineering Group Cooperation kwa awamu ya kwanza utachukua Hekta 315 ambapo zaidi wakulima 600 wanatarajia kunufaika moja kwa moja na mradi huo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.