• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

WADAU WATAKA LISHE IWE AJENDA YA KUDUMU KWENYE MIKUSANYIKO NA VIKAO

Posted on: August 11th, 2023

Wadau wa Lishe Wilayani Sengerema wamesema ili kufikia malengo ya shughuli za Lishe katika ngazi ya Halmashauri, ni vyema ajenda ya Lishe ikawa ya kudumu katika kila mikutano ya hadhara na vikao vya ndani.


Ushauri huo umetolewa leo Ijumaa Agosti 11, wakati wa kikao cha Tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe uliowakutanisha watendaji wa kata za Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na baadhi ya wakuu wa Idara na vitengo vya Halmashauri.


Wajumbe hao wamesema iwapo elimu ya Lishe itatolewa kupitia mikutano mbalimbali ya hadhara na mikusanyiko mingine kila mtu atakuwa na uelewa wa kutosha kuhusiana na masuala ya Lishe ambapo pia wameshauri watalaamu wa Lishe washirikishwe kwenye ziara za viongozi pamoja na vikao vya ngazi ya vijiji na kata kwa lengo la kutoa elimu ya Lishe.


"Suala la lishe liguse kila kiongozi, kupitia mikutano ya hadhara elimu itolewe na si kuiachia idara ya afya pekee katika utoaji wa elimu ya Lishe" ameshauri Muuguzi Mkuu wa Wilaya ndugu Charles Manyaga.


Mtendaji wa kata ya Busisi Ndugu Adam Salumu ameshauri shule zote  msingi na Sekondari kuendeleza na kuanzisha mashamba ya Viazi Lishe  shuleni ili kuongeza  huduma ya chakula shuleni ambayo itasaidia kuboresha  Lishe ya wanafunzi pamoja na kuongeza mahudhurio shuleni.


Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Ndugu Fadhili Abel ameunga mkono suala la ushirikishwaji wa wataalamu wa Lishe kwenye kila ziara za viongozi na kuzitaka shule zote za Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kuwa angalau na ekari 2 za Viazi Lishe ili kuboresha Lishe ya wanafunzi.


Awali kimkaribisha Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Dkt. Fredrick Mugarula amesema lengo la kufanya kikao cha Tathimini ya Utekelezaji wa Lishe ni pamoja na kujitathimi kulingana na Viashiria vilivyo kwenye Mkataba wa Lishe ngazi ya Halmashauri ambapo amesema Halmashauri mejipanga kuhakikisha changamoto zote zinazokabili shughuli za Lishe zinatatuliwa ili kufikia lengo.


Afisa Lishe wa Wilaya Bi. Neema Sappy amesema miongoni mwa changamoto zinazokwamisha utekelezaji wa shughuli za lishe ni pamoja na baadhi ya shule kutokutoa huduma za chakula, upungufu wa vifaa vya kutathimini Hali ya  Lishe kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano pamoja na upungufu wa chakula Dawa kwa ajili ya watoto wenye utapiamlo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA -UCHAGUZI MKUU MWAKA 2025 July 01, 2025
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • WAZIRI MKUU ASIFU MAENDELEO YA SENGEREMA

    May 19, 2025
  • DED SENGEREMA AGUSWA NA KERO ZA WATUMISHI

    May 02, 2025
  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.