Majaribio ya awali ya Mradi wa uzalishaji wa Gesi asilia kupitia ufadhiri wa shirika la United Nations Development Programme (UNDP) umeonekana kuwa na mafanikio makubwa kwa jamii ya wilaya ya Sengerema kutokana kupunguza tatizo la kukata miti ovyo na kupunguza uharibifu wa Mazingira.
Mradi huo umeingia wilayani Sengerema mnamo mwaka 2015 katika kijiji cha Nyampande wilayani hapa ambapo umeonekana kuwa na mwitikio mkubwa kwa jamii kuhitaji kutumia mradi huo.
Akizungumzia mradi huo mwezeshaji wa mradi UNDP Joseph Malkia kwa niaba ya shirika la UNDP ameeleza jinsi jamii ilivyoupokea mradi huo.
Kwa upande wake Afisa mazingira wa wilaya ya Sengerema Bwn, Ally Salim amefafanua mfumo wa mradi huo unavyofanya katika jamii .
Aidha Bwn, Salim ameongeza kuwa baada ya mradi huo kuanza wamejitahidi kutoa elimu juu ya faida ya mradi kwa jamii na kuwahidi kuwa kupitia mradi huo watalinda mazingira pamoja na kuwapa watoto na kinamama nafasi ya kuachana na utafutaji wa kuni.
Sengerema District Council
Anuani ya Posta: Box 175
Simu ya Mezani: 028 2590162
Simu: 0688223308
Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz
Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.