• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

TABASAMU AWATAKA WATUMISHI KUTATUA KERO ZA WANANCHI KWA WAKATI

Posted on: July 11th, 2024

DED, Wakuu wa Idara Watoa Somo

Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema wameaswa kufanya kazi kwa bidii sambamba na kutoa ushauri ipasavyo kwa wakuu wa idara na viongozi wengine ngazi ya Wilaya ili kuweza kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi katika ngazi za vitongoji na vijiji.


Wito huo umetolewa leo na Mbunge wa jimbo la Sengerema Mhe. Hamis Tabasamu kwenye kikao cha kazi kilichojumuisha waratibu Elimu kata, watendaji wa kata, wakuu wa shule, walimu wakuu, waganga wa wafawidhi wa vituo vya afya na zahanati kilichofanyika leo (11.07.2024) Sekondari ya Sengerema.


Akiongea na watumishi hao, Mhe. Tabasamu amesema kumekuwepo na changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema zikiwemo huduma bora  za afya na elimu hivyo amewataka watumishi hao kuhakikisha wanafanya kazi kwa bidii ili kupunguza changamoto hizo ambazo wakati mwingine wananchi wamekuwa wakiwasilisha moja kwa moja kupitia ofisi ya mbunge na yeye mwenyewe.


"Fanyeni kazi zenu kwa bidii, lakini hakikisheni pia mnatusaidia kwenye ukusanyaji wa mapato, ninyi ni maafisa wa Serikali shaurini juu ya mambo mbalimbali mnayoyaona hayaendi sawa kwenye maeneo yenu" amesema Mhe. Tabasamu.


Mapema akifungua kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Binuru Shekidele amewataka watumishi hao kufanya kazi kwa bidii na ubunifu ili kuyafikia malengo mbalimbali yaliyowekwa na Halmashauri ikiwemo usimamizi wa mapato na miradi ya maendeleo huku akisema kuwa ataendelea kuwachukulia hatua za kinidhamu watumishi wote wazembe na wale wanaokwamisha shughuli mbambali za Serikali.


Kupitia kikao hicho, wakuu wa idara na vitengo vya Halmashauri wamepata fursa ya kuelezea mipango yao ya utekelezaji wa majukumu mbalimbali katika kila idara ambayo yanawahusu watumishi hao sambamba na usimamizi wa watumishi waliopo chini yao, usimamizi wa raslimali, miradi na ukusanyaji wa mapato.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.