• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

TABASAMU AKOSHWA NA WINGI WA MIRADI SENGEREMA, AMSHUKURU RAIS SAMIA

Posted on: June 14th, 2023

Aomba Ujenzi wa Vituo vya Afya na Malambo ya Mifugo


Mbunge wa jimbo la Sengerema Mhe. Hamis Tabasamu amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema miradi mingi ya maendeleo ndani ya muda mfupi ambayo imekuwa ikitekelezwa na Serikali ya awamu ya sita.


Mhe. Tabasamu ametoa shukrani hizo wakati wa ziara ya Rais Samia Wilayani Sengerema kukagua maendeleo ya ujenzi wa daraja la Kigongo-Busisi.


Mhe. Tabasamu amesema Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema imekuwa ikipokea fedha nyingi za miradi ya maendeleo hivyo kuifanya Wilaya kupiga hatua kimaendeleo ndani ya muda mfupi.


Mhe. Tabasamu ametoa mfano wa baadhi ya sekta zilizopata fedha nyingi ni pamoja na sekta ya barabara ambapo hivi karibuni ujenzi wa barabara ya lami Sengerema - Buchosa utaanza, upandishwaji wa hadhi ya Barabara tano kwa kujengwa kwa kiwango cha moramu, kuridhiwa kwa ujenzi wa Barabara ya Kamanga- Sengerema kwa kiwango cha lami ambapo itajengwa kwa awamu na kwa kuanzia  kilometa 10 zitajengwa pamoja na uwekaji wa taa za Barabarani katika mji wa Sengerema.


Sekta zingine zilizotajwa na Mhe. Tabasamu ni pamoja na elimu ambapo zaidi ya shilingi bilioni 6 zimeletwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema na Utekelezaji wa miradi  ya Maji.


"Sengerema ni kama ndiyo imepata uhuru mhe. Rais, yaani miradi ni mingi, inazunguka kama tairi la gari" amesema mhe. Tabasamu.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewashukuru mamia ya wananchi wa Sengerema waliojitokeza kumsikiliza eneo la Busisi ambapo amesema wingi wa watu hao ni ishara kuwa wamejitokeza kumshukuru.


Mhe. Samia amesema wingi wa miradi ianyoendelea kutekelezwa wilayani Sengerema ni ukamilishaji wa ahadi zilizoachwa na Hayati Dkt. John Pombe Magufuli hivyo ameahidi kukamilisha miradi yote kwa wakati.


Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Prof. Makame Mbarawa amesema ujenzi wa daraja hilo lenye urefu wa kilometa tatu unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Februari, 2024.

Matangazo ya Kawaida

  • TAARIFA YA FEDHA YA HESABU ZA MWISHO HALMASHAURI YA WILAYA SENGEREMA KWA MWAKA ULIOISHIA TAREHE 30 JUNI 2024 August 06, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI MBALIMBALI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA SENGEREMA July 29, 2025
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MAKUBALIANO YA NYONGEZA KATI YA SERIKALI NA KAMPUNI YA NYANZAGA MINING COMPANY LIMITED KWA AJILI YA UCHIMBAJI MKUBWA WA MADINI YA DHAHABU

    August 20, 2025
  • MAADHIMISHO YA KILELE CHA JUMA LA ELIMU YA WATU WAZIMA HALMASHAURI YA WILAYA YA SENGEREMA

    August 20, 2025
  • MAFUNZO KWA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA HALMASHAURI YA WILAYA YA SENGEREMA

    August 04, 2025
  • MAADHIMISHO YA SIKU YA KUMBUKIZI YA MAUAJI YA WATU WENYE UALBINO

    July 29, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.