• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI KUENDELEA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WALIMU

Posted on: June 3rd, 2024


 *Tahadhali yatolewa juu ya Mikopo Umiza*

 *Malipo ya Uhamisho yalipwe bila upendeleo*

*Lugha mbaya kwa Walimu zakemewa*

Serikali imewahahakikishia walimu wote Wilayani Sengerema kuwa itaendelea kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili ili kuhakikisha wanafanya kazi katika mazingira mazuri.


Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Elimu kutoka Ofisi ya Rais - TAMISEMI Dkt. Emmanuel Shindika kwenye kikao cha pamoja na walimu wa shule za Msingi na Sekondari wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kilichofanyika leo (03.06.2024) Sekondari ya Sengerema.

Dkt. Shindika amesema kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa walimu ikiwemo suala la upandishwaji wa madaraja, kubadilishwa miundo, mapunjo ya mishahara, madai ya likizo, fedha za uhamisho na pamoja na lugha mbaya kwa walimu hivyo amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kukubali kutatua changamoto hizi haraka ikiwemo ulipaji wa malimbikizo ya mishahara kwa walimu pamoja na watumishi wengine.


"Katika kutatua changamoto hizi wote tumpongeze mhe. Rais Samia,  kuanzia tarehe 01.07. 2024 jumla ya walimu 54,000 watapanda madaraja kwa mserereko, kati yao 52,000 watapanda kwa utaratibu wa kawaida" amesema Dkt. Shindika.

Dkt. Shindika pia amewaasa  walimu kuona namna ya kujiongezea kipato na kuachana na mikopo umiza ambayo imesababisha walimu wengi kuwa katika matatizo kwenye maeneo ya kazi na amewataka viongozi mbalimbali kutumia lugha za staha kwa walimu na watumishi wengine pindi wanapofika ofisini kwa ajili ya kufuatilia changamoto zao.


Afisa Elimu Mkoa wa Mwanza, Martin Nkwabi amesema Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema imekuwa ikifanya vizuri kwenye taaluma pamoja na ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya sekta ya elimu.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema, Dkt. Fredrick Mugarula amesema sekta ya elimu Wilayani Sengerema imekuwa ikifanya vizuri ikiwemo suala la ufaulu kwa shule za Msingi na Sekondari kwenye mitihani ya kitaifa ambapo umekuwa ukipanda kila mwaka.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.