• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

SENGEREMA YAPONGEZWA KUPUNGUZA HOJA, HATI SAFI MFULULIZO

Posted on: June 26th, 2024

Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza, imepongezwa kwa kupunguza hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kutoka hoja 17 hadi kubaki na hoja 1 kwa mwaka 2022/2023 na kutoka hoja 22 hadi  hadi kubaki na hoja 4 zilizokuwepo kwa kipindi cha nyuma pamoja na kuendelea kupata hati safi kwa miaka mitatu mfululizo.

Pongezi hizo zimetolewa leo  (Juni 26, 2024) na Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza,  Balandya Elikana kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwenye kikao maalumu cha Baraza la Madiwani kwa ajili ya kujadili taarifa ya CAG inayoishia Juni 2023 kilichofanyika kwenye ukumbi wa Sekondari ya Sengerema.


Katibu Tawala Mkoa amesema Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kwa miaka ya iliyopita ilikuwa na hoja nyingi sana za CAG hivyo ameupongeza uongozi wa Halmashauri kwa kujibu hoja hizo na hatimaye kubakiza hoja chache ambazo nazo zinaweza kufutwa kama maoni ya mkaguzi yakifanyiwa kazi vizuri.


"Tuna hoja chache sana zilizobaki, kipindi cha nyuma kulikuwa na hoja nyingi sana mmetoa vielelezo hoja zimefutwa ninawapongeza sana kwa jitihada hizi kwani hizi hoja zinaelekea kuisha kabisa' Amesema Katibu Tawala Mkoa.


Mapema akiwasilisha taarifa ya CAG kwenye kikao hicho, Sapensia George amesema kutokana na ukaguzi uliofanyika katika kipindi kinachoishia Juni 2023 Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ilipata hati inayoridhisha ambapo pia imefanikiwa kupata hati inayoridhisha  kwa miaka mitatu mfululizo.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Sengerema, Mark Agustine Makoye ameupongeza uongozi wa Halmashauri kwa kuendelea kusimamia vyema maagizo ya Serikali ambapo imesababisha kupungua kwa hoja za CAG pamoja na kupiga hatua kwenye miradi ya maendeleo.


Mkuu wa  Wilaya ya Sengerema Mhe. Senyi Nganga amesema kumekuwepo na juhudi kubwa kutoka kwa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema katika kujibu hoja za CAG hivyo amepongeza kwa jitihada hizo sambamba na juhudi za ukusanyaji wa mapato ndani ambapo Halmashauri imefikia asilimia 86 ambapo ameiagiza Halmashauri kuendelea kupunguza madeni mbalimbali ya wazabuni wanaoidai Halmashauri.

Akifunga kikao hicho mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema, Yanga Makaga amesema kupitia kamati ya Fedha ya Halmashauri pamoja na Baraza la madiwani kwa ujumla wataendelea kuweka mikakati kwa ajili ya kudhibiti uibukaji wa hoja mpya, hivyo amewataka watumishi wa Halmashauri kuendelea kufanya kazi kwa ushirikiano.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.