• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

SENGEREMA KUNUFAIKA NA SHULE MBILI MPYA KUPITIA SEQUIP NA BOOST

Posted on: March 22nd, 2023

Halmashauri yapongezwa kusimamia vyema malengo ya BOOST na SEQUIP


Na: Richard Bagolele


Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema itanufaika na ujenzi wa shule mbili mpya za Msingi na Sekondari kupitia Mpango wa Kuimarisha na Kuboresha Elimu ya Msingi nchini (BOOST) na Mpango wa Maendeleo wa Kuboresha Elimu ya Sekondari (SEQUIP) inayofadhiliwa na Benki ya dunia.


Hayo yamebainishwa tarehe 21 Machi, 2023 na timu ya ufuatiliaji kutoka Benki ya Dunia,  TAMISEMI na Wizara ya Elimu wakati wa ziara ya siku moja ya kukagua maendeleo ya Mpango wa BOOST na SEQUIP kwa shule za Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema.


Kupitia ziara hiyo, Mkurugenzi wa Elimu ya Awali na Msingi kutoka TAMISEMI ndugu Susana Nyarubamba ameuagiza uongozi wa kata ya Misheni na Nyampulukano mahali ambapo shule hizo zinajengwa,  kuhakikisha miradi hiyo inajengwa kwa kufuata taratibu pamoja na ushirikishwaji wa wadau wote mhimu ili miradi hiyo ikamilike kwa wakati na kwa ubora uliokusudiwa.


"Niwaombe ndugu zangu tufanye kazi kwa kushirikiana pindi miradi hii itakapoanza, asiwepo mtu wa kufanya kazi peke yake, tuzingatie maelekezo bila kukiuka taratibu, tufuate miongozo na maelekezo ya Serikali, tusipunguze thamani na ubora wa miradi hii" amesisitiza ndugu Nyarubamba.


Naye mwakilishi wa Benki ya Dunia ndugu Innocent Mulindwa mbali na kupongeza usimamiaji mzuri wa malengo ya BOOST na SEQUIP ameuasa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kuhakikisha wanaunga mkono juhudi za Serikali kupitia miradi hiyo kwa kusimamia vyema miradi hiyo ili thamani ya fedha iweze kuonekana.


Awali akisoma taarifa ya Halmashauri, Mkuu wa Idara ya Elimu Msingi ndugu Donati Bunonos amesema Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema inaendelea kutekeleza mpango wa BOOST na SEQUIP kupitia mpango wa mafunzo kazini kwa walimu wote (MEWAKA), ambapo kila shule imetenga masaa mawili kwa wiki lengo ikiwa ni kujengeana uwezo na umahiri wa kufundisha mada mbalimbali za masomo zinazoonekana kuwa na changamoto.


Kupitia mradi wa SEQUIP Halmashauri pia umefanikiwa kujenga shule mpya ya Sekondari ya Ibondo na vituo viwili vya mafunzo nje ya mfumo rasmi (AEPW) pamoja na utekelezaji wa mpango wa shule salama kwa shule zote za Sekondari.


Mpango wa BOOST na SEQUIP inatekelezwa katika Halmashauri zote nchini ikiwa na lengo la kuboresha na kuimarisha miondombinu ya shule, kuboresha mafunzo kazini ya walimu, kuongeza vifaa vya kufundishia na maabara.


Timu hiyo ya ufuatiliaji  imetembelea shule ya Msingi Pambalu, Sekondari ya Ibondo, TRC Sengerema,Sekondari ya Nyampulukano, pamoja na maeneo ambapo shule mpya ya Sekondari ya kata ya Misheni itajengwa na kijiji cha Mwabayanda ambako kutajengwa shule mpya ya msingi kupitia mpango wa BOOST.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.