• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

SEKONDARI MPYA 11 SENGEREMA KUANZA JANUARI 2024

Posted on: July 23rd, 2024

Ukarabati wa shule 7 za Msingi kukamilika


Jumla ya shule mpya 11 za Sekondari zinazoendelea kujengwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema zinatarajiwa kukamilika mwezi Agosti 2024 na kuanza kutumika Januari 2025.


Akikagua maendeleo ya ujenzi wa shule hizo pamoja na ukarabati wa shule za msingi leo (Julai 23, 2024), Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema, Binuru Shekidele amesema kukamilika kwa shule kutasaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani sambamba na kupunguza umbali kwa wanafunzi waliokuwa wanasoma mbali ambapo kukamilika kwa shule hizo kutapunguza tatizo la umbali pamoja na utoro kwa wanafunzi.


Miongoni mwa shule zilizotembelewa ni pamoja na ujenzi wa Sekondari mpya ya Sogoso iliyopo kata ya Sima, na Igaka kata ya Buzilasoga ambazo zinatarajiwa kukamilika mwezi Agosti 2024 ambapo kukamilika kwa shule hizi kutaifanya Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kuwa na shule 46 za Sekondari.


Shule zingine mpya za Sekondari ambazo zinaendelea kukamilishwa ni pamoja na Igulumuki, Isole, Chamabanda, Busulwangili, Kagunga, Nyitundu, Balatogwa, Kabusuri na Ilekanilo ambazo zinajengwa kwa fedha za Serikali kuu na baadhi kwa kushirikiana na Mamlaka ya Elimu Tanzania.


Aidha katika ziara hiyo Mkurugenzi Mtendaji aliyeambatana na baadhi ya wakuu wa idara, waamekagua maendeleo ya ukamilishaji wa madarasa katika Sekondari ya Ibisabageni, shule ya msingi Sogoso na Pambalu ambazo zimepata fedha kutoka Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA).


Katika ziara hiyo Mkurugenzi alipata nafasi ya kuongea na walimu wa Sekondari ya Ibisabageni ambapo amepongeza uongozi wa shule hiyo kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa miundombinu ya shule hiyo ambapo pia amewataka walimu shuleni hapo kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuinua kiwango cha taaluma katika shule za Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema.


Kupitia kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji amewaahidi watumishi wakiwemo walimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema wenye sifa na vigezo vya kupanda madaraja watapanda bila kuwepo na upendeleo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • WAZIRI MKUU ASIFU MAENDELEO YA SENGEREMA

    May 19, 2025
  • DED SENGEREMA AGUSWA NA KERO ZA WATUMISHI

    May 02, 2025
  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.