• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

RC MALIMA ATIMIZA AHADI YAKE KWA WANANCHI WA MAMI

Posted on: March 8th, 2023

Mkuu wa Wilaya atoa siku 5 wazazi kupelekea watoto shule


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Kigoma Malima ametimiza ahadi  yake ya fedha taslimu na mifuko 20 ya Saruji kwa wananchi wa kijiji cha Mami kilichopo kata ya Kishinda Wilayani hapa.


Akikabidhi fedha hizo shilingi laki 7 (laki 5 za Mkuu wa Mkoa, laki 1 kutoka ofisi ya Mkuu wa Wilaya na laki 1 kutoka kwa mdau wa maendeleo wa Kishinda) leo tarehe 08 Machi, 2023 kwa wananchi hao, Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Senyi Ngaga amewapongeza wananchi hao kwa kujitolea kuchangia nguvu kazi kwenye miradi mbalimbali ambapo amesema kwa kufanya hivyo kutasaidia miradi inayopelekwa katika eneo hilo kukamilika pasipokuwa na migogoro.


"Hiki mnachokifanya cha kujitolea ni kitu kizuri sana na cha kuigwa, ukichangia kwenye miradi ya maendeleo unakuwa na uchungu na mradi huo kwa sababu umechangia na mradi utauthamini" amesema Mkuu wa Wilaya.


Kwa upande mwingine Mkuu wa Wilaya ametoa siku 5  kwa mtendaji wa kata ya Kishinda kuhakikisha anawakamata wazazi wa watoto wote ambao hawajajiunga kidato cha kwanza  katika shule za Sekondari Kishinda na Tunyenye akishindwa kufanya hivyo hatua kali zitachukuliwa kwa mtendaji huyo.


Diwani wa kata ya Kishinda Mhe. Vicent Shokolo ameipongeza Serikali kwa kupeleka miradi mingi katika kata hiyo ambapo amemhakikishia Mkuu wa Wilaya ya Sengerema kuwa, miradi yote itakayopelekwa katika kata hiyo wananchi wapo tayari kuchangia nguvu kazi kwani wanathamini jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali katika kupeleka miradi ya maendeleo katika kata hiyo.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Binuru Shekidele amewapongeza wananchi wa kijiji cha Mami kwa kujitolea kuchimba mtaro kwa ajili ya kupeleka maji katika zahanati ya kijiji hicho ambapo amewaomba kuendelea na moyo huo wa kujitolea kwa miradi mingine.


Akiwa katika ziara yake Wilayani hapa tarehe 1 Machi, 2023 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima aliahidi kuchangia shilingi laki 5 kwa ajili ya chakula cha wananchi wa kijiji cha Mami waliojitolea kuchimba mtaro wa kupitisha bomba la maji linalopeleka maji kwenye zahanati ya kijiji cha Mami pamoja na mifuko 20 ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Mami.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI March 14, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI KADA YA DEREVA II NA MTUNZA KUMBUKUMBU II November 11, 2022
  • Majina ya walioitwa kwenye Mafunzo ya Ukarani, Tehama na Usimamizi wa Maudhui katika Sensa ya Mwaka 2022 July 26, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili wa Kazi ya Afisa Mtendaji wa Kijiji Daraja III, Katibu Muhtasi Daraja III na Dereva Daraja II July 05, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI SENGEREMA LAKOSHWA NA UKUSANYAJI WA MAPATO

    March 15, 2023
  • DC SENGEREMA AKEMEA MMOMONYOKO WA MAADILI

    March 08, 2023
  • RC MALIMA ATIMIZA AHADI YAKE KWA WANANCHI WA MAMI

    March 08, 2023
  • BUYAGU KUWA KITUO CHA MFANO KILIMO CHA PAMBA

    March 02, 2023
  • Ona vyote

Video

RC ATOA SIKU NNE WAZAZI KUPELEKA WATOTO KIDATO CHA KWANZA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.