• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

RC MALIMA ATAKA UWEPO WA MAJI YA UHAKIKA KWENYE VITUO VYA AFYA, SHULE SENGEREMA

Posted on: March 1st, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wilayani hapa kuhakikisha huduma za Maji ya uhakika zinapatikana kwenye vituo vyote vya kutolea huduma za afya pamoja na taasisi zote za elimu ili kupunguza adha kwa watoa huduma, wagonjwa, wanafunzi wa bweni pamoja wananchi wanaozunguka taasisi hizo.


Akikagua maendeleo ya Ujenzi wa Kituo cha afya Kanyelele kilichopo kata ya Buzilasoga kinachotarajiwa kuhudumia zaidi ya wananchi 1852 chini ya Mpango wa kunusuru Kaya Masikini (TASAF III) kwa zaidi ya Milioni 543, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amesema huduma za afya haziwezi kutolewa pasipo kuwepo na huduma ya maji ya uhakika hivyo ameagiza kutengwe fedha ili kuchimba kisima kirefu kitakachosaidia kituo hicho pindi kitakapo anza kutoa huduma pamoja na wananchi wanaozunguka eneo hilo.


"Kituo cha Afya bila huduma za maji haiwezekani na tusidanganyane na kutegemea Chanzo cha Maji ya mvua badala yake naomba Halmashauri itenge angalau Milioni 30 hapa ili tupate kisima kirefu cha Maji kwenye kituo hiki." Amesema mhe. Malima.


Aidha, mhe. Malima ameuagiza uongozi wa Halmashauri kuona namna kuongeza muda wa kufanya kazi na wafanyakazi kwenye kituo hicho ili kiweze kukamilika ifikapo  Machi 15, 2023  ambapo amesema kukamilika kwa wakati kwa mradi huo pamoja na mingine ya TASAF kutasaidia kutimiza vigezo vya kuendelea kupata ufadhili wa miradi mingine ya maendeleo.


Mratibu wa TASAF wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ndugu Malisa Ndugha amesema ujenzi wa kituo hicho cha Afya Kanyelele umefikia Asilimia 80 na kinatarajiwa kuukamilika ifikapo Machi 10, 2023.


Miradi mingine iliyotembelewa na Mkuu wa Mkoa ni pamoja na Zahanati ya Mami,  Shamba la mkulima mwezeshaji wa Pamba la ndugu Maneno Lukubanija wa Buyagu, Ukaguzi wa eneo la makazi ya wananchi watakaopisha eneo la Mgodi wa Nyanzaga, ujenzi wa vyumba saba vya madarasa Sekondari ya Ngoma pamoja na mkutano wa hadhara na wananchi wa Ngoma.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI March 14, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI KADA YA DEREVA II NA MTUNZA KUMBUKUMBU II November 11, 2022
  • Majina ya walioitwa kwenye Mafunzo ya Ukarani, Tehama na Usimamizi wa Maudhui katika Sensa ya Mwaka 2022 July 26, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili wa Kazi ya Afisa Mtendaji wa Kijiji Daraja III, Katibu Muhtasi Daraja III na Dereva Daraja II July 05, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI SENGEREMA LAKOSHWA NA UKUSANYAJI WA MAPATO

    March 15, 2023
  • DC SENGEREMA AKEMEA MMOMONYOKO WA MAADILI

    March 08, 2023
  • RC MALIMA ATIMIZA AHADI YAKE KWA WANANCHI WA MAMI

    March 08, 2023
  • BUYAGU KUWA KITUO CHA MFANO KILIMO CHA PAMBA

    March 02, 2023
  • Ona vyote

Video

RC ATOA SIKU NNE WAZAZI KUPELEKA WATOTO KIDATO CHA KWANZA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.