• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

RC MAKALLA AWATAKA WATENDAJI SERIKALINI KUSHIRIKIANA NA VIONGOZI WA KISIASA

Posted on: June 5th, 2023

Asisitiza nidhamu kazini na Ukusanyaji wa Mapato


Na: Richard Bagolele - Sengerema



Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Amos Makalla amewataka watumishi wa Serikali Wilayani Sengerema kufanya kazi kwa kushirikiana na viongozi wa kisiasa ili kuharakisha maendeleo.


Mhe. Makalla ametoa agizo hilo leo wakati wa ziara ya kujitambulisha wilayani hapa ambayo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, dini, wazee maarufu, wafanyabiashara pamoja na watumishi wa umma.


Mhe. Makala amesema kufanya kazi kwa ushirikiano na uwepo wa mahusiano mazuri baina ya watumishi na viongozi wa kisiasa husaidia kuondoa migogoro kazini na migawanyiko, hivyo ni vyema kila mmoja athamini uwepo wa mwingine kwani lengo ni kuleta maendeleo kwa wananchi.


"Sisi wote lengo letu ni kuijenga Sengerema kwa umoja wetu, watendaji  toeni ushirikiano kwa madiwani na viongozi wengine wa siasa vile vile wanasiasa fanyeni hivyo kwa watumishi, ili tusonge mbele kwani sisi wote tunategemeana na tunatekeleza Ilani moja" amesisitiza Mhe. Makalla.


Kwa upande mwingine Mhe. Makalla amewataka watumishi wa umma wilayani hapa kufanya kazi kwa nidhamu ikiwemo matumizi mazuri ya muda, huduma bora kwa wananchi na utatuaji kero mbalimbali za wananchi kwa wakati.


Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Senyi Ngaga amesema Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema inayo miradi mingi ambayo inaendelea kutekelezwa ikiwemo ya sekta ya elimu na afya hivyo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa wingi wa miradi ambapo amesema kukamilika kwa miradi hiyo kutaifanya Sengerema kuwa ya mfano kwa maendeleo.


"Sisi tunamshukuru sana Mhe. Rais, tuna miradi mingi ambayo inakwenda kuifungua Sengerema kama vile mradi wa Daraja la Kigongo-Busisi, Barabara ya lami Sengerema - Buchosa, Mgodi wa Nyanzanga ambapo kukamilika kwake kutaiweka Sengerema kwenye sehemu ya juu sana na tutahakikisha tunaimarisha makusanyo ya mapato ya ndani" amesema Mhe. Ngaga.


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Sengerema Mhe. Augustine Makoye amesema Wilaya ya Sengerema inayo imani kubwa na ujio wa Mhe. Amos Makalla hivyo amemhakikishia ushirikiano wa hali ya juu katika kuchochea maendeleo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.