• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

RC MAKALLA AMALIZA MGOGORO WA ENEO LA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI NYAMPULUKANO- SENGEREMA

Posted on: November 9th, 2023

Aaagiza ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ya Nyampulukano uanze kwa kasi kwani serikali ilishatoa fedha Milioni 200


Aagiza pia shule mpya ya SEQUIP ujenzi uendelee haraka

Aagiza Mwezi Januari shule zote mpya zitakazojengwa zianze kutoa huduma

Awataka watendaji na viongozi kushirikiana  kuchapa kazi na kusahau msuguano wa nyuma

Atangaza kuanza rasmi kwa utoaji wa huduma hospitali ya Wilaya ya Mwabaluhi

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amemaliza rasmi mgogoro uliodumu kwa zaidi ya miezi Sita wa wapi ujenzi wa shule mpya ya Sekondari chini ya Mradi wa Uboreshaji wa Elimu (SEQUIP) wapi ijengwe.


Mhe. Makalla ametatua mgogoro huo wakati akiongea na wananchi wa kata ya Nyampulukano eneo la FDC mlimani ambapo kabla ya kufika hapo alitembelea maeneo yote mawili yaliyopendekezwa kujengwa kwa shule hiyo mpya ya SEQUIP.


Mkuu wa mkoa amesema, kutokana na mgogoro huo kudumu kwa muda mrefu, serikali ya awamu ya sita imeona ni vyema kujenga shule mpya katika maeneo yote mawili ya Misheni na Nyampulukano ili huduma hiyo muhimu iwafikie wote.


"Serikali imetoa shilingi milioni 200 kwa ajili ya kukamilisha Miundombinu ya madarasa iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi wakati huohuo shule mpya ya SEQIP itaendelea kujengwa katika eneo lililopendekezwa lililopo kata ya Misheni." Makalla.


Vilevile, amewataka Halmashauri ya wilaya ya sengerema kuongeza kasi ya ujenzi wa shule hizo na kwa pamoja ifikapo mwezi januari 2023 zianze kutoa huduma kwa wananchi kwani wamesubiri kwa muda mrefu.


"Mimi kama Mtendaji mkuu nakushukuru sana Mhe. Mkuu wa mkoa maana tulishakwama kutokana na sintofahamu ya wapi tutajenga shule pamoja na kupokea fedha za ujenzi huo, nakuahidi mwezi januari shule hii itaanza na sasa tunafanya kazi kwa kasi", amesema Mkurugenzi Mtendaji, Binuru Shekidele.


Naye, Diwani kata ya Misheni Mhe. Francis Majumba amefafanua kuwa wananchi wa kata hiyo imepata faraja kutokana na kutatuliwa kwa kitendawili hicho na kupatikana kwa suluhu ambayo inakuja kuwatatulia adha ya kusuasua kwenye maendeleo kwenye eneo la Elimu.


Mapema asubuhi Mkuu wa Mkoa aliliagiza Shirika la Umeme wilaya Sengerema (TANESCO) kupeleka umeme kwenye shule mpya ya msingi ya Kijiweni iliyojengwa kwa zaidi ya shilingi Milioni 540 kwenye kata ya Chifunfu ambayo inakuja kuondoa kero ya msongamano wa wanafunzi kwenye shule mama ya Bugumbikiso.


Vilevile, amemtaka Mkandarasi anayejenga jengo la makao makuu ya Halmashauri ya Sengerema kukamilisha ujenzi huo ifikapo mwezi Mei 2024 kwa mujibu wa mkataba ili huduma zianze kutolewa hapo.


Halikadharika, amewakaribisha wananchi wa wilaya hiyo kupata huduma za afya zinazotolewa kwenye hospitali mpya ya wilaya hiyo iliyojengwa kwa zaidi ya Bilioni 2.8 na ameahidi kuwasiliana na mamlaka husika ili ziletwe Bilioni 1.5 za kukamilisha ujenzi kwenye hospitali hiyo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.