• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

RC MAKALA AWATAKA WATENDAJI WA KATA SENGEREMA KUTATUA KERO ZA WANANCHI KWA WAKATI

Posted on: November 15th, 2023
  1. Ataka watenge siku maalumu kusikiliza Kero za wananchi

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewaagiza watendaji wa kata Wilayani hapa kutenga siku ya Alhamisi ya kila wiki kwa ajili ya kutatua kero na kushughulikia malalamiko mbalimbali yanayowakabili wananchi ili kupunguza kero hizo kwa wakati badala ya kusubiri viongozi wa kitaifa.


Mhe. Makala ametoa agizo hilo leo Novemba 08, 2023 alipokuwa kwenye mkutano wa kusikiliza malalamiko na utatuaji wa kero mbalimbali za wananchi wa Wilaya ya Sengerema mkutano uliofanyika kwenye viwanja vya stendi ya zamani mjini Sengerema ambao umedhuriwa na wananchi mbalimbali pamoja na viongozi wa mbalimbali wa Serikali.


Mhe. Makalla Amewataka watendaji wa kata kutenga siku maalumu ya kusikiliza kero za wananchi katika ngazi ya kata ili kupunguza malalamiko kwa viongozi mbalimbali wanapotembelea Wilayani hapa.


Amesema kutokana na ongezeko la malalamiko yanayohusiana na ardhi Wilayani Sengerema ni ishara ya udhaifu wa watendaji katika kutatua malalamiko ya wananchi katika eneo husika.


"Watendaji wa kata, punguzeni matatizo ya ardhi ya mashamba, tengeni siku moja ya wiki watangazieni wananchi waje waeleze kero zao" amesema Mhe. Makalla.


Mhe. Makalla ametoa siku 14 kwa viongozi wa  Wilaya ya Sengerema kuhakikisha wanajibu utekelezaji wa  maelekezo yote yalitolewa kupitia mkutano huo ambapo wananchi 63 walitoa malalamiko yao.


Mapema akimkaribisha Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Senyi Ngaga amesema ataendelea na mikutano ya kusikiliza kero za wananchi katika ngazi za kata na ameahidi kushughulikia kero zote zilizowasilishwa kupitia mkutano huo.


Huu ni mwendelezo wa mikutano ya usikilizaji na utatuaji wa kero za wananchi katika ngazi za Wilaya unaofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla ambapo kwa siku ya alhamisi Novemba 09, 2023 Mkuu wa Mkoa atakagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.