• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

MIUNDOMBINU BORA YA KISASA SEKONDARI ZA SENGEREMA KIVUTIO WANAFUNZI KIDATO CHA TANO

Posted on: August 18th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Senyi Ngaga amesema uwepo wa miuondombinu bora na ya kisasa kwenye shule za Sekondari za Sengerema kunaiafanya Wilaya ya Sengerema kuwapokea wanafunzi wote 720 wa kidato cha tano waliopangiwa Wilayani hapa na njia pekee ya kumshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa miundombinu hiyo ni pamoja na wanafunzi hao kupata matokeo mazuri kwenye mitihani ya kitaifa.


Mkuu wa Wilaya ameyasema hayo siku ya Ijumaa agosti 18, 2023 kwenye hafla ya kuwakaribisha wanafunzi wa kidato cha tano waliopangiwa Wilayani Sengerema iliyofanyika shule ya Sekondari Sengerema.


Mkuu wa Wilaya amesema Serikali ya awamu ya sita imekuwa ikitekeleza miradi mingi ya Maendeleo hususan kwenye sekta ya elimu hivyo amesema namna pekee na nzuri ya kumshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kusoma kwa bidii na kufaulu vizuri kwenye mitihani ya kitaifa.


"Ndani ya miaka miwili Wilaya ya Sengerema tumepokea fedha zaidi ya bilioni 10 kwenye sekta ya elimu, haya yote yanafanyika ili kuwatengenezea mazingira mazuri ninyi wanafunzi, na njia pekee ya kumshukuru Mhe. Rais ni ninyi kupata divisheni one nyingi kweye mihani wa kidato cha sita" amesema Mkuu wa Wilaya.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema amesema kufuatia matokeo mazuri ya kidato cha sita 2023, yameifanya shule ya Sekondari Sengerema kuwa ni shule ya mfano mkoani Mwanza hivyo amewaandoa hofu wanafunzi waliopangiwa shuleni hapo na Nyampulukano Sekondari kuripoti kwa wakati kwani shule zinao walimu wazuri na miundombinu bora ya kufundishia na kujifunzia hivyo hakuna sababu ya wanafunzi hao kutokufaulu vizuri.


Ndugu Shaban Lupogo mmoja ya wazazi aliyesindikiza mwanafunzi aliyepangiwa shuleni hapo kutoka Mkoani  Rukwa amesifu ubora wa miundombinu iliyopo shule Sekondari Sengerema ambapo amewaomba  wanafunzi waliopangiwa shuleni hapo kuhakikisha wanaripoti kwa wakati kwani shule hiyo inayo mandhari mazuri na amesifu ufaulu mzuri wa shule hiyo.


Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Bi. Genoveva Chuchuba amesema kwa Halmashauri ya Sengerema kati ya wanafunzi 592 waliopangiwa katika shule za Sengerema na Nyampulukano hadi kufikia siku ya Ijumaa Agosti 18, 2023 zaidi ya wanafunzi 335 sawa na asilimia 56 wameripoti katika shule hizo.


Jumla ya wanafunzi 720 wamepangiwa kujiunga kidato cha tano kupitia shule za Sengerema na Nyampulukano zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema na Nyehunge iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa hadi kufikia Ijumaa agosti 18, 2023 jumla ya wanafunzi 393 sawa na asilimia 54.5 wameripoti katika shule hizo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.