• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

MILIONI 73 ZA MIKOPO ISIYO NA RIBA ZANUFAISHA VIKUNDI 19 SENGEREMA

Posted on: January 17th, 2023

Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza kupitia fedha za mapato ya ndani imetoa Mkopo wa Shilingi Milioni 73 kwa vikundi 19 vya Wanawake shilingi milioni 42.5, Vijana shilingi milioni 25 na Wenye ulemavu shilingi milioni 6.5 vinavyojishughulisha na shughuli mbalimbali za ujasiriamali.


Akifungua mafunzo kwa vikundi vilivyonufaika na Mkopo huo leo (jumanne tarehe17 Januari, 2023) ndugu Boniphace Kasasiro kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji amesema mikopo hiyo isiyo na riba imetolewa na Halmashauri kwa vikundi hivyo kwa kufuata vigezo vyote, hivyo amewaomba wanavikundi hao kwenda kuitumia vyema kama ikivyokusudiwa na iweze kutimiza malengo ya wanavikundi hao.


"Tunavyo vikundi vingi vilivyosajiliwa katika Halmashauri yetu ambavyo viliomba Mkopo huu, hivyo ni vyema na ninyi mkirejesha mikopo hii kwa wakati ili vikundi vingine pia viweze kunufaika kama ninyi" amesema ndugu Kasasiro


Mapema akimkaribisha Mkurugenzi Mtendaji kwenye mafunzo hayo, Mwenyekiti wa jukwaa la Wanawake Sengerema Bibi Daling Matonange ameishukuru Halmshauri ya Wilaya ya Sengerema kwa kuongeza kiwango cha mkopo kwa vikundi hivyo ukilinganisha na kipindi kilichopita ambapo itavisaidia vikundi hivyo kufikia malengo na ndoto zao za kuwa wafanyabiashara wakubwa pamoja na kuzalisha bidhaa zenye ubora wa hali ya juu.


Baadhi ya wanavikundi walionufaika na mkopo huo wameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kwa kutoa mikopo hiyo sambamba na kuwapa mafunzo ya namna bora ya kutumia fedha hizo kwani hapo awali waliogopa kuchukua mikopo hiyo kutokana na kutokuwa na elimu ya uelewa hivyo mafunzo hayo yatawasaidia kusimamia vyema fedha hizo pamoja na kufanya marejesho kwa wakati.


"Nimepata Mkopo kwa mara ya kwanza, kwa kiasi kikubwa  mkopo huu umenimeongezea mtaji wangu ambao ulikuwa kidogo sana" amesema ndugu Sanifu Tanzania ambaye ni mnufaika kupitia kundi la wenye ulemavu.


Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kwa mwaka wa fedha 2022/2023 imepanga kutoa mikopo isiyokuwa na riba zaidi ya shilingi milioni 176 itokanayo na asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa vikundi mbalimbali vya wanawake, vijana na wenye ulemavu.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.