• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

MIAKA 61 YA UHURU, SENGEREMA YAJIVUNIA NA MAENDELEO LUKUKI

Posted on: December 9th, 2022


Wananchi wilayani Sengerema mkoani Mwanza wametakiwa kujivunia kwa maendeleo yaliyopatikana wilayani humo ukilinganisha na kabla ya uhuru ambapo kulikuwa na changamoto nyingi za kimaendeleo.

Hayo yameelezwa leo na Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Senyi Ngaga wakati wa maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru yaliyofanyika sekondari ya Sengerema ambapo pia yameenda sambamba na kongamano la wazi lililowashirikisha viongozi mbalimbali wa serikali, madhehebu ya dini, wazee maarufu na wananchi wa Sengerema.

Mhe. Ngaga amesema kabla ya Uhuru Wilaya ya Sengerema haikuwa na shule ya sekondari lakini kwa sasa kuna shule za sekondari 43, shule za msingi zilikuwa 22 lakini kwa sasa kuna shule za msingi 110.

Ameongeza kusema Serikali imeendelea kutekeleza miradi mikubwa ikiwemo ile ya sekta za Nishati, Maji, afya, barabara na maendeleo ya jamii.

"Tunayo miradi mingi mikubwa ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa nchini kote,  ikiwemo ndani ya Wilaya yetu, ikiwemo daraja la Busisi, daraja hili likikamilika litapunguza kero nyingi, haya ndiyo maendeleo tuliyokuwa tunatafuta baada ya kupata uhuru, tuna kila sababu ya kumpongeza Mhe Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan." amesisitiza Mhe. Ngaga.

Meneja wa wakala wa Barabara za vijijini na mijini (TARURA) Wilaya ya Sengerema mhandisi Prosper Francis  amesema kabla ya uhuru Wilaya ya Sengerema haikuwa na mtandao wa barabara unaoeleweka bali kulikuwa na njia ndogo ndogo za waenda kwa miguu lakini kwa sasa Wilaya  Sengerema ina mtandao wa barabara zenye urefu wa kilomita 2,709.

Meneja Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wilaya ya Sengerema Mhandisi Musa Bujiku amesema hapo awali maji katika mji wa Sengerema yalikuwa yanatoka kwa mgao kwa sasa Wilaya inajivunia kwa kupata miradi mingi ya maji ambapo amesema kwa mwaka huu wa fedha serikali imetoa kiasi cha bilioni 47 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maji ambayo inatarajiwa kukamilika mwaka 2023 ambapo upatijanaji wa maji vijijini utapanda kutokana asilimia 57  asilimia 85.

Maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru yamefanyika Sekondari ya Sengerema na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na madhehebu ya dini pamoja na wananchi.

Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni Miaka 61 ya Uhuru, Amani na Umoja ndiyo nguzo ya maemdeleo yetu.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.