• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akipokea taarifa fupi juu ya mradi wa Maji kabla ya kufanya uzinduzi katika kijiji cha Nyamazugo

Posted on: July 5th, 2017

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amewataka wananchi wa Sengerema na mkoa wa Mwanza kwa ujumla kulinda na kutunza ziwa Victoria kwa kukomesha uvuvi haramu katika ziwa hilo.

Rais ameyasema hayo wakati akizindua mradi mkubwa wa maji na usafi wa Mazingira uliogharimu fedha za kitanzania zipatazo Bil. 22.4 Wilayani Sengerema mkoani hapa.

Mh. Rais, amesema nilazima suala la uvuvi haramu likemewe kwa nguvu zote na kwa ngazi zote, “Nimeambiwa wapo baadhi ya watu kwa kushirikiana na watumishi wa umma wasio wa aminifu wanaendesha uvuvi haramu, nitoe wito kwa yeyote atakaye bainika kufanya hivyo, serikali haitakuwa na msamaha kwake” alisema Mh. Rais.

Rais Magufuli amesema, mtu anapotumia sumu ziwani anauwa hata viumbe visivyo husika na zaidi sana dawa zinazotumika kusafisha maji hazina uwezo wakuondoa kemikali, hivyo nilazima kila mwananchi aelewe kutumia sumu ya thiodani ziwani ni hatari kwa maisha yao.

Ameongeza kuwa, kukamilika kwa mradi huo ni kukamilisha aliyo ahidi katika kampeni zake wakati akiomba kura ambapo, kwa sasa wananchi wa Sengerema watapata maji kwa asilimia 100.

Kwa upande wake, Waziri maji Mhandisi Gerson Lwenge, amesema mradi huo wenye uwezo wa kuzalisha lita milioni 15.84 na kunufaisha wakaazi wapatao 138,000 wa mji wa Sengerema na vijiji vya jiarani vya Nyamazugo, Kijuka, Mwaliga na Nyamizeze kwa asilimia 100 hadi kufikia mwaka 2030.

Awali akitoa salaam za Mkoa wa Mwanza, Mkuu wa mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella, amesema mka huo kwa sasa umjipanga kikamilifu kwenye mageuzi ya Mapinduzi ya viwanda, huku akimakikishia Mh. Rais uwepo wa Viwanda 12 vikubwa ambavyo vipo tayari kwakufunguliwa.

Aidha mkuu huyo wa mkoa alisema, mkoa umeamua kuweka nguvu kubwa katika zao la Pamba, ‘Mh. Rais katika Msimu wa 2016/2017 mavuno yetu ya Pamba yalifikia tani Mil.5, lakini katika msimu huu, tunatazamia kupata sio chini ya tani Mil. 20.

Naye Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja, akishukuru kwa niaba ya wananchi wa Sengerema alisema, wanamshukuru sana Mh. Rais kwakuendelea kuwatumikia watanzania kwa moyo wa uaminifu lakini zaidi sana kukamilisha ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa vitendo inayo himiza kuwa na maji safi na salama kwa Vijijini kwa asilimia 85 na mijini asilimia 95,

“Mh. Rais yawezekana ni kweli wananchi wa Sengerema waliteseka kwa muda mrefu, lakini sisi wanasiasa yawezekana tulikuwa na shida kubwa zaidi, maana mradi huu umekuwa wa muda mrefu na mahali pengine hata tulipokuwa tukiongewa walikuwa hawatuelewi majukwaani” alisema Ngeleja.

Kuzinduliwa kwa mradi mkubwa wa maji katika Mji wa Sengerema na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli ni ishara kwamba Mji wa Sengerema sasa utapata maji kwa asilimia miamoja ambapo wananchi wapatao 138,000 watanufaika na mradi huo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.