• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

MGODI WA NYANZAGA WAKAMILISHA UJENZI WA MADARASA NA OFISI SEKONDARI MPYA LUBUNGO

Posted on: September 27th, 2023

Waahidi kutengeneza Madawati 160 na kutoa miche ya Miti

Jamii Wilayani Sengerema imeaswa kuithamini na kuitunza miradi mbalimbali iliyopo katika maeneo yao ili iweze kudumu na kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Wito huo umetolewa leo tarehe 27 Septemba, 2023 na Katibu Tawala Wilaya ya Sengerema Ndugu Cuthbert Midala kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya katika Hafla ya kukabidhi vyumba vinne vya Madarasa na ofisi mbili za walimu zilizojengwa kwa ushirikiano wa wananchi na kampuni ya Sotta Mining inayojishughulisha na uchimbaji wa Dhahabu katika Mgodi wa Nyazanga Hafla iliyofanyika kijiji cha Lubungo kata ya Igalula.

Amesema kumekuwa na miradi mingi inayotekelezwa na Serikali lakini imekuwa ikitelekezwa na jamii hivyo amewaasa wananchi hao kuhakikisha wanailinda vyema miradi hiyo ili iweze kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Katibu Tawala amempongeza Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mhe. Mbunge wa Sengerema Hamis Tabasamu, Kampuni ya Sotta Mining na Wananchi wa Lubungo kwa kufanikisha ukamilishaji wa miundombinu hiyo.

"Miundombinu hii tusipoitunza tutakuwa tumejiadhibu sisi wenyewe maana ipo hapa kwa ajili yetu hivyo tuilinde kwa nguvu zote" amesisitiza Katibu Tawala Wilaya ya Sengerema.

Mkuu wa kampuni ya Sotta Mining ndugu Isaack Lupokela amesema katika kuboresha elimu, wadau mbalimbali wanayo nafasi kubwa kufanikisha, hivyo Sotta Mining imeona ni vyema ishirikiane na wananchi kupitia sekta ya elimu kwani ni jukumu linalogusa kila mdau wa maendeleo.

Amewaasa wananchi wa Lubungo kuhakikisha wanapeleka watoto shule kwani ndiyo haki yao msingi sambamba na kufuatilia maendeleo ya wanafunzi hao.

Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari ndugu Genoveva Chuchuba ameishukuru kampuni hiyo na wananchi kwa ujenzi wa vyumba vya madarasa na ofisi ya walimu ambapo amewaomba wazazi kijijini hapo kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika malezi ya watoto pamoja na kupeleka watoto katika shule hiyo ikiwa ni sehemu ya shukrani kwa kampuni hiyo. Amesema kukamilika kwa shule hiyo kutasaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi Sekondari ya Ngoma yenye jumla ya wanafunzi 1,220.
 
Akisoma taarifa ya ujenzi wa mradi huo, Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Sotta Mininng ndugu Bwana amesema ujenzi wa mradi huo umejengwa kwa ushirikiano na wananchi ambapo ukamilishaji wa ujenzi madarasa hayo umejengwa kikundi cha wajasiriamali kilichopo Kijiji cha Ngoma kwa gharama ya shilingi milioni 38.

Diwani wa kata ya Igalula Mhe. Faustine Shibiliti ameishukuru kampuni ya Sotta Mining  kwa ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa na ofisi mbili za walimu ambapo amesema  kukamilika kwa shule hiyo kutasaidia kupunguza utoro na na mimba kwa wananfunzi kike hasa katika vijiji vya Lubungo na Nyasigu ambapo kuna umabali wa kilometa 8 kufika Sekondari ya Ngoma. Mhe. Shibiliti ameiomba kampuni hiyo kuwezesha pia upatikanaji wa madawati pamoja na vyoo katika shule hiyo ili iweze kuanza kwa wakati.

Matangazo ya Kawaida

  • TAARIFA YA FEDHA YA HESABU ZA MWISHO HALMASHAURI YA WILAYA SENGEREMA KWA MWAKA ULIOISHIA TAREHE 30 JUNI 2024 August 06, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI MBALIMBALI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA SENGEREMA July 29, 2025
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MAKUBALIANO YA NYONGEZA KATI YA SERIKALI NA KAMPUNI YA NYANZAGA MINING COMPANY LIMITED KWA AJILI YA UCHIMBAJI MKUBWA WA MADINI YA DHAHABU

    August 20, 2025
  • MAADHIMISHO YA KILELE CHA JUMA LA ELIMU YA WATU WAZIMA HALMASHAURI YA WILAYA YA SENGEREMA

    August 20, 2025
  • MAFUNZO KWA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA HALMASHAURI YA WILAYA YA SENGEREMA

    August 04, 2025
  • MAADHIMISHO YA SIKU YA KUMBUKIZI YA MAUAJI YA WATU WENYE UALBINO

    July 29, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.