• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

KAMATI YA SIASA MKOA YAKOSHWA NA MIRADI SENGEREMA

Posted on: May 22nd, 2024

Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mwanza imeridhishwa na ubora wa miradi mbalimbali ya Maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ambapo pia wameitaka Halmashauri ya Sengerema kuongeza kasi ya ujenzi wa Jengo la Utawala ili lianze kutumika.


Akiongea wakati wa ziara hiyo leo (22.05.2022), Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Michael Lushinge (smart) amesema ubora wa miradi hiyo unatokana na usimamizi mzuri chini ya uongozi wa Mkuu wa Wilaya, Halmashauri na CCM Wilaya ya Sengerema ambapo ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema hivyo amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda kwa usimamizi mzuri wa miradi hiyo.


"Miradi hii tuliyoitembelea leo ina thamani kubwa ikikamilika italeta manufaa makubwa kwa wananchi wetu,  hivyo tunampongeza sana Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuamua fedha hizi zije zitekeleze miradi hii Sengerema" amesema Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza.


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amepongeza jitihada za Wilaya za kuwaletea wananchi maendeleo ambapo pia amesema kukamilika kwa ujenzi  uwanja wa mpira wa Miguu utakuwa ni wa manufaa kwa wananchi na ujenzi wa uwanja huo ni miongoni mwa vipaumbele vya Serikali ya awamu ya sita hivyo ameahidi kuleta timu ya Pamba jiji na timu zingine za ligi kuu ili uwanja huo utumike kama chachu kwa vijana wa Sengerema.


Mkuu wa Mkoa amepongeza usimamizi mzuri wa miradi ya Maendeleo ya Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ambapo amesema kwa sasa miradi ya Sengerema inakamilika kwa ubora na kwa wakati.


Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Sengerema, Mark Agustine Makoye amesema kujengwa kwa uwanja wa mpira wa miguu wa Mnadani ni ishara ya uwepo wa viongozi wazuri katika Wilaya, hivyo amempongeza Mkuu wa Wilaya, Mwenyekiti wa Halmashauri na Mbunge wa jimbo la Sengerema kwa kuja na wazo la ujenzi wa uwanja huo ambao pia ni chanzo cha mapato ya Halmashauri.


Miradi iliyokaguliwa na Kamati ya Siasa Mkoa wa Mwanza ni pamoja na mradi wa Maji Nyasigu- Lubungo - Ngoma kata ya Igalula, Ujenzi wa daraja la Bugakara, Jengo la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema, Ujenzi wa jengo la Mamlaka ya Mapato Wilaya ya Sengerema na Ujenzi wa uwanja wa Michezo Mnadani yote ikiwa na jumla ya bilioni 20.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.