• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

KAMATI YA FEDHA SENGEREMA YAPONGEZA SHIRIKA LA CEDAR KUNUSURU KITUO CHA AFYA KAMANGA

Posted on: November 12th, 2024



Mapato ya Ndani Kukamilisha Ujenzi wa Madarasa Kamanga na Ofisi ya Kata Ibondo


Bilioni 1.3 Kukamilisha Jengo la Utawala Machi 2025


Na; Richard Bagolele- Sengerema


Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema imelipongeza shirika la CEDAR kutoka Australia kwa ufadhili wa ujenzi wa ukuta wa kuzuia maji kutoka ziwa Viktoria pamoja na jitihada za shirika hilo kukiimarisha kituo cha afya Kamanga.


Shukrani hizo zimetolewa leo Novemba 12, 2024 na wajunbe wa kamati hiyo wakati wa ziara ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kwa kipindi cha  Julai hadi Septemba 2024.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Mhe. Yanga Makaga ambaye pia ni diwani wa kata Nyamatongo amelishukuru shirika hilo kwa ufadhili wa mara kwa mara pamoja na ujenzi wa ukuta huo ambapo amesema kujengwa kwake kutakinusuru kituo hicho ambacho kimekuwa kikiathiriwa na maji ya Ziwa Viktoria na kusababisha kusitishwa kwa huduma pamoja na kuathiri makazi ya watumishi wa kituo hicho.


"kujengwa kwa ukuta huu kutasaidia sana kukinusuru kituo hiki  kujaa maji mara kwa mara kutoka ziwani, ujenzi huu ni wa gharama kubwa bila ninyi Halmashauri tusingeweza kujenga ukuta huu kwani ni gharama kubwa" amesema Mwenyekiti wa Halmashauri.


Akiwasilisha taarifa ya ujenzi wa ukuta huo unaojengwa pembezoni mwa ziwa Viktoria, Msimamizi wa ujenzi kutoka shirika hilo, Musa Victor amesema utekelezaji wa mradi huo ilianza mwezi Oktoba 2024 na unatarajiwa kukamilika mwezi Januari 2025 kwa gharama za shilingi milioni 266 mradi unaojengwa na kampuni ya SIMR kutoka jijini Mwanza.


Miradi mingine iliyokaguliwa na Kamati hiyo ni pamoja na Ujenzi wa madarasa mawili na ofisi shule ya Msingi Kamanga kwa gharama ya shilingi milioni 25 fedha za mapato ya ndani ambapo wajumbe wamepongeza kamati ya ujenzi ya kijiji cha Kamanga  kwa kufanikisha ujenzi huo vizuri na thamani ya fedha kuonekana. Kamati hiyo pia imekagua ujenzi wa ofisi  ya Mtendaji wa Kata ya Ibondo unaojengwa kwa gharama ya shilingi milioni 15 fedha kutokana na mapato ya ndani.


Kamati hiyo pia imekagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la Utawala lililoko Bomani ambalo liko katika hatua za upauaji na linatarajiwa kukamilika mwezi Machi 2025 ambapo mwezi Oktoba 2024, Serikali imetoa kiasi cha shilingi Bilioni 1.3 kwa ajili ya ukamilishaji wa jengo hilo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.