• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

ISUNGANG'OLO KUANZA MHULA WA JULAI NA MIUNDOMBINU MIPYA

Posted on: June 30th, 2023

Madarasa Mapya 14 yenye Madawati, Jengo la Utawala na Matundu ya Vyoo kukamilika punde

Shule ya Msingi Isungang'olo iliyopo kata ya Nyatukala Wilayani hapa inatarajiwa kukamilisha ujenzi wa miundombinu mipya kabla ya mhula wa pili wa masomo unaotajiwa kuanza mapema mwezi Julai 2023.


Akikagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali shuleni hapo leo Juni 30, 2023 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Binuru Shekidele ameiagiza kamati ya ujenzi ya shule hiyo kuhakikisha miundombinu yote inakamilika kwa wakati kwa kuzingatia viwango.


"Simamieni ukamilishaji huu vizuri, msimamieni fundi akabidhi madarasa yaliyojengwa vizuri na yakamilike mapema zaidi"  amesisitiza Mkurugenzi Mtendaji.


Mkuu wa Idara ya Elimu Msingi ndugu Donati Bunonosi amesema jumla   ya madarasa 14 yenye madawati, jengo la utawala na matundu ya vyoo 11 vimejengwa shuleni hapo kwa gharama za shilingi 450,500,000 fedha kutoka Serikali Kuu Mfuko wa Maafa.


Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bi. Getruda Malisa amesema shule hiyo ina jumla ya wanafunzi 1,013 ambao wamekuwa wakitumia madarasa machache kutokana na baadhi ya madarasa ya shule hiyo kuezuliwa na Mvua kubwa mwezi Novemba 2022.


Mwanafunzi Dotto Ramadhani anayesoma darasa la nne katika shule hiyo amempongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuamua kupelekea fedha kujenga miundombinu mipya shuleni hapo ambapo amesema kukamilika kwa vyumba hivyo vya madarasa kutasaidia sana kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani.


Shule ya Msingi Isungang'olo ilikumbwa na maafa mnano mwezi Novemba 2022 na kusababisha baadhi ya madarasa shuleni hapo kuezuliwa na mengine kubomoka. Serikali kupitia mfuko wa Maafa mwezi Aprili 2023 ilitoa kiasi cha shilingi 450,500,000 kwa ajili ya ujenzi wa Miundombinu mipya shuleni hapo ambapo ujenzi umefikia zaidi ya asilimia 90.


Miradi mingine iliyotembelewa na Mkurugenzi Mtendaji ni pamoja na ujenzi wa shule mpya ya Msingi Nyatukala kupitia mradi wa BOOST kwa gharama ya shilingi 540,300,000, na ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa shule ya Msingi Pambalu kwa gharama ya shilingi milioni 50 fedha za mapato ya ndani.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.