• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri ya Sengerema

Posted on: July 23rd, 2019

Hadi kufikia mwaka wa fedha 2019/2020 Halmashauri ya Sengerema imeweza kutekeleza miradi mbalimbali ya maendelea kwa wananchi wake kwa kiwango cha hali ya juu.

1. Mwaka huu wa fedha 2019/20 halmashauri ya Sengerema ni miongoni mwa halmashauri 27 tu nchini tuliotengewa fedha za kujenga hospitali ya wilaya. Kwa hiyo Sengerema tutakuwa na hospitali 2 za hadhi ya Wilaya (yaani ya Mission na hiyo ya Serikali itakayojengwa).

2. Tumefanikisha ujenzi wa vituo vya afya Kagunga, Katunguru na Kamanga tulichosaidiwa na wafadhili. Na bado mipango inaendelea kwa kata zingine na zahanati kwa kila kijiji. Shukrani sana kwa ushiriki wa wananchi.

3. Barabara za Sengerema - Nyanchenche - Ngoma A na ile ya Sima - Ikoni tumefanikiwa kuzipandisha hadhi, sasa zinahudumiwa na Tanroads hili nalo ni bao la kisigino.

4. Barabara ya Kamanga-Sengerema - Taratibu zote za maandalizi ya awali zimekamilika kuijenga kwa lami. Serikali inajipanga kulipa fidia kwa watakaoathirika na kutangaza tenda ya ujenzi.

5. Maji:

(a) Sengerema mjini tatizo tulishalitatua.

(b) Kwa sasa Serikali, kupitia Mamlaka ya Maji Mza (MWAUWASA) wanashughulikia ununuzi wa  mabomba na vifaa vingine kwa ajili ya ujenzi wa busta pale Mission ili kutatua kero ya maji Mission na Kizugwangoma.

(c) MWAUWASA pia anashughulikia ununuzi wa mabomba kwa ajili ya Ibondo kwa Mwarabu na Zanzibar Mwabaluhi.

(d) MWAUWASA pia anasimamia shoo ya mradi wa Nyampande ambapo mkandarasi yupo site.

(e) Hivi karibuni tenda kwa ajili ya kufikisha maji Sima kutoka Sengerema mjini itatangazwa. Shoo hii pia itasimamiwa na MWAUWASA.

(f) MWAUWASA huyo huyo ndiyo anayesimamia mradi wa maji Nyasigu - Lubungo - Ngoma A wanakamilisha taratibu za uhakiki wa kitaalamu kabla ujenzi haujaanza.

(g) Tukikamilisha mradi wa maji Sima, tutaanza mradi wa maji Balatogwa - Tunyenye.

(h) Mradi wa maji kwa kata zote zinazopakana na ziwa Victoria-Kasenyi, Chifunfu, Katunguru, Nyamatongo, Ngoma, Kahumulo, Kasungamile, Busisi, Buyagu na Igalula.

-Dizaini na taratibu zingine za  kitaalamu kuhusu maandalizi ya mradi huu             zimeishakamilika Serikali inaandaa tenda kwa ajili ya kupata mkandarasi.

(g) Miradi ya visima nayo inaendelea katika baadhi ya maeneo.

(k) Maji Kang'washi na Mwaliga. Tunasubiri fedha zitoke tukamilishe maboresho ya upatikanaji wa maji katika maeneo haya.

6. Umeme - Mkandarasi yupo jimboni anaendelea kwa maeneo ambayo hayajafikiwa, jimbo ni kubwa ila atamaliza tu, tuvumilie.

7. Ukamilishaji wa maboma yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi.

-Serikali imeahidi kutoa fedha  kuyakamilisha, tuvute subra.

8. Ujenzi wa stendi mpya Bukala:

-Halmashauri tunaendelea kukusanya fedha ili tukamilishe ujenzi huu.

9. Tumefanikiwa kujenga sekondari kila kata.

10. Barabara za Sengerema - Nyehunge na Katunguru - Nyamazugo:

Zimo kwenye mpango wa kujengwa kwa lami.

11. Daraja la Kigongo - Busisi

-Tenda imeishatangazwa.

12. Mgodi wa Dhahabu Ngoma:

-Serikali imeahidi kutoa leseni ya uchimbaji kwa mwekezaji ndani ya mwaka  huu wa fedha 2019/20.

-Leseni ikitoka ndiyo ujenzi wa mgodi uanze. Kwa hiyo uchimbaji unaweza kuanza mwaka 2021.

13. Fedha za Mfuko wa Jimbo - Huwa tunapata sh 60 milioni tu kwa mwaka. Matumizi yake ni kama tulivyokubaliana katika vikao vya Madiwani lengo ikiwa ni;

 - kuimarisha barabara ambazo hazina bajeti ya Tarura.

14. TARURA

-Wanaendelea kujenga barabara kwa kadri ya upatikanaji wa fedha kutoka Serikalini.

-TARURA pia anawajibika kuongeza mtandao wa lami kwa barabara za mjini Sengerema. Tutashirikiana nao kufanikisha lengo hili.

15. MICHEZO

Baada ya kupunguza kero ya maji na kupata fedha za hospitali mpya ya wilaya, sasa tunaanza kujielekeza kwenye uimarishaji wa michezo na ujenzi wa uwanja wa michezo mjini Sengerema. Tataendelea kuwajulisha hatua kwa hatua.

16. Busisi - Buyagu - Ngoma A road

-Tunaendelea kufuatilia ahadi ya Mhe Rais kuijenga barabara hii kwa lami.

17. Mradi wa maji Buyagu-Kalangalala-Bitoto:

-Uko kwenye hatua za mwisho kukamilika.

18. Chuo Kikuu Buyagu

-Ujenzi wa Chuo Kikuu hiki cha Kilimo Buyagu/Isole unaendelea vizuri kwa ufadhili wa Wakorea.

19.RUZUKU KWA KAYA MASIKINI.

-Halmashaur ya Sengerema kupitia Mfuko Wa Maendeleo ya Jamii(Tasaf)Imetoa ruzuku ya fedha kwa kaya masikini zaidi 6963.Jumla ya Tsh 968,736,000.00

-Wapendwa haya ni baadhi tu ya mambo tuliyofanya na tunayoendelea kuyafanya.

“Anayepuuza apuuze, ila sisi tunasonga mbele”

&

Sengerema ni yetu sote, tuendelee kuijenga kwa pamoja

                                               

Julai, 2019

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.