Akitoa taarifa hiyo mratibu wa Magonjwa ya mlipuko katika Halmashauri ya wilaya ya Sengerema Bw. Mgonja amewataka wajumbe kuchukua tahadhari mbalimbali za kujikinga dhidi ya Mlipuko wa ugonjwa huo hatari wa Homa Kali ya Mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona (COVID - 19)
Akitoa msisitizo alisema, "nawaomba ndugu zangu elimu hii tunayopeana hii leo ni kwa ajili ya kupeana uelewa ili tunapokutana na jamii huko katika maeneo yetu tukasaidie kuelimisha na siyo kuitia hofu jamii" Wakichangia wajumbe mada hiyo waliuomba uongozi wa Halmashauri na wilaya uendelee kutoa elimu kwa umma hasa maeneo ya vijijini kwani bado uelewa dhidi ya ugonjwa huu ni mdogo hasa maeneo ya pembezoni mwa mji.
Nae mwenyekiti wa kamati hiyo Dkt. Emmanuel Kipole ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Sengerema aliyekuwa amewakilishwa na Ndg. Allan Agustine ambaye ni Katibu Tawala alipokuwa akifunga kikao hicho amewaomba wazazi na walezi pamoja na viongozi wa dini kuhakikisha wanakuwa msitari wa mbele katika kutoa elimu juu ya ugonjwa huu hatari kwa waumini wao.
Sengerema District Council
Anuani ya Posta: Box 175
Simu ya Mezani: 028 2590162
Simu: 0688223308
Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz
Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.