• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

'DIVISHENI ONE' 400 SENGEREMA SEKONDARI ZAWAKOSHA WAKUU WA IDARA

Posted on: July 21st, 2023

Kifuatia baraza la mitihani kutangaza matokeo ya kidato cha sita 2023, na sekondari ya Sengerema kufanya vizuri kwenye matokeo hayo imebainika kuwa umoja na ushirikiano baina ya walimu, Idara ya Elimu Sekondari na Menejimenti ya Halmashauri ndiyo siri ya mafanikio hayo.


Hayo yamebainishwa leo wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza walimu hao iliyohudhuriwa na kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri Bi. Genoveva Chuchuba pamoja na Mkuu wa Idara ya Utumishi na Utawala Bi. Christina Bunini.


Akiongea na walimu hao, Mkuu wa Idara ya Utumishi ameupongeza uongozi wa shule hiyo kwa matokeo mazuri waliyopata na kuwataka walimu hao waongeze juhudi zaidi.


"Na mimi kama afisa Raslimali watu mmenipaisha sana, naomba juhudi hizi ziendelee, Sengerema Sekondari mmefanya vizuri sana kila mtu anataka kuleta mtoto shuleni hapa" amesema Ndugu Bunini.


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Bi. Genoveva Chuchuba ambaye ni Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari amesema matokeo hayo mazuri yamechangiwa na maadili mazuri ya walimu wa shule hiyo hivyo amewataka kuendeleza nidhamu hiyo kwani ndiyo msingi wa mafanikio.


Mkuu wa shule ya Sekondari Sengerema Ndugu Zacharia Kahema ameushukuru uongozi wa Halmashauri na Idara ya Elimu Sekondari kwa ushirikiano anaoupata kutoka kwao ambapo amesema lengo la shule ni kupata ufaulu wa daraja la kwanza tu ikitokea bahati mbaya iwe wachache daraja la pili.


Kwa mujibu wa matokeo yalitangazwa  Julai 13, 2023 na Baraza la Mitihani nchini (NECTA) Sekondari ya Sengerema iliyokuwa na wanafunzi 679 waliosajiliwa kufanya mtihani, wanafunzi 408 walipata daraja la kwanza, wanafunzi 263 daraja la pili na watano daraja la tatu.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.