• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

DC SENGEREMA AWATAKA WATOTO KUSEMA HAPANA KUZUIA UKATILI

Posted on: June 16th, 2023

Watoto watoa tahadhari matumizi ya Mitandao

Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Senyi Ngaga amewataka watoto wilayani hapa kujifunza kusema hapana kwenye matukio yanayosababisha ukatili dhidi ya watoto katika jamii.


Mkuu wa Wilaya ametoa agizo hilo leo kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika yaliyofanyika kiwilaya kata ya Sima na kuhudhuriwa na mamia ya watoto na wananchi wa kata hiyo na maeneo ya jirani.


Mkuu wa Wilaya amesema matukio mengi ya ukatili dhidi ya watoto yamekuwa yakitokea kipindi cha likizo hivyo amewataka watoto hao kutimiza wajibu wao kwa kukemea na kupinga matendo ya ukatili kwa kutumia elimu ya kujitambua wanayoipata shuleni kwani matukio mengi ya ukatili yanatokea kwa sababu watoto wenyewe kukubali  kutendewa tofauti na matukio ya ubakaji.


"Na ninyi wenyewe mjifunze kusema hapana kwenye matendo ya ukatili,  Mkifungua shule, takwimu zinaonesha mimba zimekuwa zikiongezeka, mtoto wa Sekondari unapataje mimba? ni uzembe na kukosa nidhamu" amesema mkuu wa Wilaya.


Mkurugenzi Mtendaji wa  Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Binuru Shekidele amesema malezi mazuri ya watoto hutoa viongozi na wananchi wazuri hivyo ameiasa jamii kuwalea watoto katika misingi ya maadili mema.


Wakisoma risala kwa Mkuu wa Wilaya, watoto hao wamewaasa watoto wengine wilayani hapa na Tanzania kwa ujumla kuchukua tahadhali dhidi ya matumizi ya mitandao ya kijamii na vifaa vya kielektroniki kwani matukio mengi ya ukatili yamekuwa yakifanyika na kuonekana kupitia mitandao hiyo hivyo wameoimba jamii na Serikali  kuwakinga watoto hao dhidi ya vitendo vya ukatili mitandaoni kwani watoto ndiyo wamekuwa waathirika wakubwa.



Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika hufanyika kila tarehe 16 mwezi Juni kutokana mauaji ya watoto yaliyofanywa na askari wa utawala wa Makaburu katika Kitongoji cha Soweto nchini Afrika Kusini tarehe 16 Juni, 1976. Mauaji hayo yalitokea wakati Askari hao wanazuia maandamano ya watoto waliokuwa wanapinga mfumo wa elimu ya kibaguzi iliyokuwa unatolewa na Utawala wa Makaburu. Katika kukumbuka siku hii, Umoja wa Nchi za Afrika mnamo mwaka 1991 uliweka Azimio la kuifanya siku ya tarehe 16 Juni ya kila mwaka kuwa siku maalum ya kuwaenzi mashujaa watoto waliokufa kwa ajili ya kudai haki yao ya kuendelezwa kielimu bila ubaguzi na hivyo kuitwa Siku ya Mtoto wa Afrika


Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni mwaka 2023 *“Zingatia Usalama wa Mtoto katika Ulimwengu wa Kidijitali*”

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.