• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

DC SENGEREMA AKEMEA MMOMONYOKO WA MAADILI

Posted on: March 8th, 2023

Asisitiza Wanawake kuungana kujikwamua kiuchumi

Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Senyi Ngaga amekemea tabia ya baadhi ya wazazi kujiweka kando kwenye malezi ya watoto kitendo kinachosababisha kushuka kwa maadili katika jamii.


Mhe. Ngaga ametoa angalizo hilo kwenye maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika kiwilaya kwenye viwanja vya stendi ya zamani mjini Sengerema na kuhudhuriwa na mamia ya wanawake.


Mhe. Ngaga amesema wakinamama wanalo jukumu kubwa la malezi majumbani lakini kutokana na kujihusisha na shughuli mbalimbali za kiuchumi na uzalishaji mali wamesahau kujihusisha na malezi hivyo amewataka wanawake hao kutimiza majukumu yao ikiwemo kufuatilia mienendo ya watoto wawapo majumbani na mahali pengine.


"Tunajukumu kubwa la malezi ndugu zangu, ni lazima tufuatilie watoto wetu wanakutana na changamoto gani kila siku, ni lazima tufuatilie na tujue watoto wetu wanakoenda wanakutana na changamoto gani?" amesisitiza Mkuu wa Wilaya.


Aidha Mhe. Mkuu wa Wilaya amewaasa wazazi kuwa makini na matumizi ya Teknolojia kwa watoto kwani mmomonyoko wa maadili kwa kiasi kikubwa umechangiwa na matumizi mabaya ya Teknolojia ikiwemo matumizi ya simu janja kwa watoto.


Katika upande mwingine Mkuu wa Wilaya amewataka wanawake wilayani Sengerema kuhakikisha wanashirikiana katika kuinua vipato vyao kupitia fursa mbalimbali zinazotolewa na Serikali hususan mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kupitia Halmashauri za Wilaya kwa kuanzisha viwanda vidogo vidogo vyenye lengo la kuwakwamua wanawake kupitia vikundi mbalimbali.


Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ndugu Christina Bunini akimkaribisha Mkuu wa Wilaya amewaasa wanawake hao kuhakikisha wanatimiza majukumu ya malezi ya watoto majumbani ili kuwa na jamii yenye maadili kwani akina mama wanayo nafasi kubwa ya kusimamia malezi bora katika ngazi ya familia.


Mapema akitoa taarifa ya  maadhimisho hayo ndugu Boniphace Kasasiro amesema lengo la maadhimisho ya wanawake duniani ni pamoja na kufanya tathimini ya shughuli mbalimbali zinazofanywa na akina mama pamoja na kubaini changamoto mbalimbali zinazowakabili wanawake.


Mwenyekiti wa Jukwaa la wanawake Wilayani Sengerema ndugu Daling Matonange ameiomba Serikali kupitia Halmashauri kuweza kuongeza kiwango na wigo wa mikopo kwa Burundi vya wanawake kwani vipo vikundi vingi ambavyo vinazalisha bidhaa mbalimbali ambavyo hukabiliwa na changamoto za kukosa mikopo hiyo.

Matangazo ya Kawaida

  • TAARIFA YA FEDHA YA HESABU ZA MWISHO HALMASHAURI YA WILAYA SENGEREMA KWA MWAKA ULIOISHIA TAREHE 30 JUNI 2024 August 06, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI MBALIMBALI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA SENGEREMA July 29, 2025
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MAKUBALIANO YA NYONGEZA KATI YA SERIKALI NA KAMPUNI YA NYANZAGA MINING COMPANY LIMITED KWA AJILI YA UCHIMBAJI MKUBWA WA MADINI YA DHAHABU

    August 20, 2025
  • MAADHIMISHO YA KILELE CHA JUMA LA ELIMU YA WATU WAZIMA HALMASHAURI YA WILAYA YA SENGEREMA

    August 20, 2025
  • MAFUNZO KWA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA HALMASHAURI YA WILAYA YA SENGEREMA

    August 04, 2025
  • MAADHIMISHO YA SIKU YA KUMBUKIZI YA MAUAJI YA WATU WENYE UALBINO

    July 29, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.