• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

DC SENGEREMA AKEMEA MMOMONYOKO WA MAADILI

Posted on: March 8th, 2023

Asisitiza Wanawake kuungana kujikwamua kiuchumi

Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Senyi Ngaga amekemea tabia ya baadhi ya wazazi kujiweka kando kwenye malezi ya watoto kitendo kinachosababisha kushuka kwa maadili katika jamii.


Mhe. Ngaga ametoa angalizo hilo kwenye maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika kiwilaya kwenye viwanja vya stendi ya zamani mjini Sengerema na kuhudhuriwa na mamia ya wanawake.


Mhe. Ngaga amesema wakinamama wanalo jukumu kubwa la malezi majumbani lakini kutokana na kujihusisha na shughuli mbalimbali za kiuchumi na uzalishaji mali wamesahau kujihusisha na malezi hivyo amewataka wanawake hao kutimiza majukumu yao ikiwemo kufuatilia mienendo ya watoto wawapo majumbani na mahali pengine.


"Tunajukumu kubwa la malezi ndugu zangu, ni lazima tufuatilie watoto wetu wanakutana na changamoto gani kila siku, ni lazima tufuatilie na tujue watoto wetu wanakoenda wanakutana na changamoto gani?" amesisitiza Mkuu wa Wilaya.


Aidha Mhe. Mkuu wa Wilaya amewaasa wazazi kuwa makini na matumizi ya Teknolojia kwa watoto kwani mmomonyoko wa maadili kwa kiasi kikubwa umechangiwa na matumizi mabaya ya Teknolojia ikiwemo matumizi ya simu janja kwa watoto.


Katika upande mwingine Mkuu wa Wilaya amewataka wanawake wilayani Sengerema kuhakikisha wanashirikiana katika kuinua vipato vyao kupitia fursa mbalimbali zinazotolewa na Serikali hususan mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kupitia Halmashauri za Wilaya kwa kuanzisha viwanda vidogo vidogo vyenye lengo la kuwakwamua wanawake kupitia vikundi mbalimbali.


Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ndugu Christina Bunini akimkaribisha Mkuu wa Wilaya amewaasa wanawake hao kuhakikisha wanatimiza majukumu ya malezi ya watoto majumbani ili kuwa na jamii yenye maadili kwani akina mama wanayo nafasi kubwa ya kusimamia malezi bora katika ngazi ya familia.


Mapema akitoa taarifa ya  maadhimisho hayo ndugu Boniphace Kasasiro amesema lengo la maadhimisho ya wanawake duniani ni pamoja na kufanya tathimini ya shughuli mbalimbali zinazofanywa na akina mama pamoja na kubaini changamoto mbalimbali zinazowakabili wanawake.


Mwenyekiti wa Jukwaa la wanawake Wilayani Sengerema ndugu Daling Matonange ameiomba Serikali kupitia Halmashauri kuweza kuongeza kiwango na wigo wa mikopo kwa Burundi vya wanawake kwani vipo vikundi vingi ambavyo vinazalisha bidhaa mbalimbali ambavyo hukabiliwa na changamoto za kukosa mikopo hiyo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI March 14, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI KADA YA DEREVA II NA MTUNZA KUMBUKUMBU II November 11, 2022
  • Majina ya walioitwa kwenye Mafunzo ya Ukarani, Tehama na Usimamizi wa Maudhui katika Sensa ya Mwaka 2022 July 26, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili wa Kazi ya Afisa Mtendaji wa Kijiji Daraja III, Katibu Muhtasi Daraja III na Dereva Daraja II July 05, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI SENGEREMA LAKOSHWA NA UKUSANYAJI WA MAPATO

    March 15, 2023
  • DC SENGEREMA AKEMEA MMOMONYOKO WA MAADILI

    March 08, 2023
  • RC MALIMA ATIMIZA AHADI YAKE KWA WANANCHI WA MAMI

    March 08, 2023
  • BUYAGU KUWA KITUO CHA MFANO KILIMO CHA PAMBA

    March 02, 2023
  • Ona vyote

Video

RC ATOA SIKU NNE WAZAZI KUPELEKA WATOTO KIDATO CHA KWANZA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.