• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

CHUO KIKUU ARDHI KUANZISHA 'KAMPASI' SENGEREMA

Posted on: July 5th, 2023

Ujenzi Kuanza Mwezi Septemba 2023 kwa gharama ya sh. Bilioni 18


Na: Richard Bagolele - Sengerema


Chuo Kikuu cha Ardhi chenye makao makuu yake jijini Dar es Salaam kinatarajia kuanza ujenzi wa tawi jipya katika kijiji cha Karumo kata ya Nyamatongo wilayani Sengerema.


Akiongea wakati wa ziara ya siku moja wilayani hapa tarehe 5 Julai, 2023 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Adolf Mkenda amesema kuanzishwa kwa tawi la chuo kikuu cha Ardhi mkoani Mwanza hususan wilayani Sengerema kutanufaisha wananchi wengi wa kanda ya Ziwa kupitia elimu itakayotolewa chuoni hapo ambayo italenga kutatua changamoto mbalimbali hususan katika maeneo ya ardhi, ujenzi na uvuvi hivyo amewaomba wananchi wa kanda ya ziwa kuchangamkia fursa chuo hicho kitakapoanza.


Katika hatua nyingine Mhe. Prof. Mkenda amewapongeza viongozi na wananchi wa Sengerema wakiongozwa na Mbunge Hamisi Tabasamu kwa utayari wa kutoa eneo kwa ajili ya ujenzi wa chuo kikuu hicho lakini pia kwa kuwa mstari wa mbele kuchangia katika miradi ya maendeleo hususan ujenzi wa vyumba vya madarasa.


"Niwapongeze wananchi wa Sengerema kwa utayari wenu wa kutoa eneo hili kwa ujenzi wa chuo, lakini pia kwa utayari wenu wa kuchangia katika miradi mbalimbali ya maendeleo, hii ni wilaya ya mfano" amesema Prof. Mkenda


Mapema akitoa taarifa ya ujenzi wa chuo hicho, Makamu Mkuu wa Chuo cha Ardhi Prof. Evaristo Liwa amesema ujenzi wa chuo hicho utaanza mapema mwezi Septemba 2023 na unatarajiwa kukamilika mwezi Novemba 2024 kwa gharama ya shilingi bilioni 18 ikijumuisha ujenzi, vifaa vya kufundishia na kujifunzia.


Prof. Liwa amesema kwa kuanza chuo hicho kitafundisha masomo ya teknolojia ya ujenzi, utaalamu wa michoro ya ujenzi, utawala wa ardhi na mazingira hususan raslimali za ziwa Victoria ambapo amesema masomo hayo yote yatatolewa kwa ngazi stashahada (Diploma) ambapo chuo kitaanza na idadi ya wanachuo 350 kwa mwaka wa kwanza.


Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Senyi Ngaga amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia chuo hicho kujengwa wilayani Sengerema ambapo amesema kujengwa kwa chuo hicho kutaisaidia Wilaya ya Sengerema kukua zaidi kiuchumi.


Akiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Mhe. Prof. Mkenda ametembelea chuo cha Maendeleo ya wananchi Karumo, chuo cha ufundi Sengerema kilichopo Nyatukala ambapo uongozi wa Wilaya umeomba kukabidhi chuo hicho Wizara ya Elimu kiweze kuwa chuo cha VETA na Tabaruka ambapo uongozi wa Wilaya umeomba ujenzi wa shule mpya ya ufundi.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.