• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

CHITANDELE KUNUFAIKA NA NYUMBA ZA WALIMU KUPITIA TASAF

Posted on: January 27th, 2023

Shule shikizi ya Chitandele iliyopo kata ya Chifunfu imeanzisha ujenzi wa nyumba moja ya familia mbili (two in one) kwa ajili ya walimu wa shule Hiyo inayojengwa kwa ufadhili wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kwa kwa kushirikiana na wananchi waliopo kisiwani humo.


Akiongea na wananchi mara baada ya zoezi la uchimbaji wa msingi wa nyumba hiyo, Diwani wa kata ya Chifunfu mhe. Robert Madaha amewaomba wananchi hao kujitoa kikamilifu kwa kushiriki katika ujenzi wa nyumba hiyo kwa kuchangia nguvu kazi ili nyumba hiyo ukamilike kwa wakati na walimu waweze kuishi karibu na shule hiyo.


"Tumepata bahati ya kuletewa mradi huu wa nyumba katika eneo letu, ni jambo jema kwetu hatuna budi kujitolea kwa nguvu kazi ili tukamilishe kwa wakati.


Akiongea kwa niaba ya Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri, Ndugu Neema Sagwa amewapongeza wananchi hao kwa kujitolea nguvu kazi ambapo amesema kuongeza kwa miundombinu katika shule hiyo shikizi kutasaidia kupata vigezo kwa ajili ya kuisajili na kuwa shule kamili ya msingi hivyo amewaomba wazazi wa eneo hilo kuhakikisha wanaandikisha watoto wote waliofikisha umri wa kwenda shule.


Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ndugu Malisa  Ndugha amesema ujenzi wa nyumba hiyo unatarajiwa kugharimu kiasi cha shilingi 68,760,943 fedha kutoka TASAF pamoja na nguvu za wananchi zinazokadiriwa kufikia shilingi milioni 6. Ndugu Malisa mesema ujenzi wa nyumba hiyo unatarajiwa kukamilika ifikapo Aprili 30, 2023 hivyo amewaomba wananchi hao pamoja na kamati ya ujenzi kuhakikisha wanatanguliza uzalendo kwanza katika shughuli za ujenzi wa nyumba hiyo.


Shule shikizi ya Chitandele ina jumla ya wanafunzi 100 wa darasa la awali hadi la nne, wanafunzi 13 wa darasa la tano hadi la saba waishio kisiwani humo hulazimika kwenda kusoma shule ya msingi Lukumbi iliyopo nje ya kisiwa hicho.


Kukamilika kwa nyumba hiyo kutaisadia shule hiyo shikizi  hiyo kuwa na nyumba 2 za walimu ambapo kwa sasa kuna nyumba moja ya mwalimu.


Kisiwa cha Chitandele kilichopo kijiji cha Lukumbi kata ya Chifunfu  kinakadiriwa kuwa kaya 76 na wakazi 300.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.