• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

BUYAGU KUWA KITUO CHA MFANO KILIMO CHA PAMBA

Posted on: March 2nd, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amepania kuboresha kilimo cha zao la Pamba ambapo ameagiza kuanzishwa kwa umoja wa wakulima wa Pamba Buyagu Wilayani Sengerema ili kuongeza uzalishaji na kutoa elimu kwa wakulima wa maeneo mengine.


Akizungumza na baadhi ya wakulima wa Pamba wa kata ya Buyagu alipotembelea  mashamba yao ya Pamba, Mhe. Malima amesema bado wakulima wa zao hilo hawalimi kilimo cha kisasa kitendo ambacho kinarudisha nyuma uzalishaji wa zao hilo, ambapo amesema mpango wa kuanzisha kilimo cha kisasa cha zao hilo utaenda sambamba na kuongeza uzalishaji wa zao hilo ili watu wengine kutoka maeneo mengine wajifunze.


"Mimi ninataka wakulima wengine kutoka maeneo yote ya Afrika waje wajifunze Buyagu kilimo bora cha Pamba na inwezekana" amesisitiza mhe. Malima



Mkuu wa Mkoa ameiagiza Bodi  ya Pamba kushirikiana na Halmashauri kuanzisha umoja wa wakulima wa Pamba wa eneo hilo pamoja na kujenga kituo maalumu cha wakulima wa Pamba kwa ajili ya kuwahudumia wakulima hao kitendo ambacho kitapelekea wakulima kuweza kukopeshwa Pembejeo.


"Mimi nawaomba, tutenge kanda hii iwe ya majaribio kwenye zao la Pamba. Tutafanya usajili wa wakulima wote, lazima tupime pia udongo huu tujue ni mbolea gani inahitajika" amesema mhe. Malima


Mhe. Malima amesema mpango huo pia utahusisha utoaji wa mikopo ya Pembejeo kwa kushirikiana na mabenki pamoja na Halmashauri kuwezesha miundombinu ya umwagiliaji pamoja na elimu ya upandaji kwa kuzingatia kanuni bora za kilimo ili mkulima kwa hekari moja apate kilo angalau 2000.


Mkuu wa Mkoa amesikitishwa kutokana na kuwaona wakulima wakipoteza fursa ya kupata fedha nyingi kupitia zao la Pamba kutokana na kutokuzingatia kanuni bora za kilimo cha Pamba.


Mkuu wa Mkoa ameunda kamati maalumu inayohusisha wataalamu wa kilimo ngazi ya Wilaya na Mkoa ambapo itaandaa taarifa mhimu za wakulima hao pamoja na ukubwa wa mashamba yao.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA -UCHAGUZI MKUU MWAKA 2025 July 01, 2025
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • WAZIRI MKUU ASIFU MAENDELEO YA SENGEREMA

    May 19, 2025
  • DED SENGEREMA AGUSWA NA KERO ZA WATUMISHI

    May 02, 2025
  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.