• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

BARAZA LA MADIWANI SENGEREMA LAWASHUKIA WAKANDARASI UKWEPAJI USHURU WA HUDUMA

Posted on: August 23rd, 2024

Latoa Siku 7 kwa Kampuni hizo Kulipa


Kamati ya Ufuatiliaji Madai Yaundwa


Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema limetoa siku saba kuanzia Agosti 23, 2024 kwa wakandarasi, wazabuni, kampuni wafanyabiashara mbalimbali wanaofanya kazi kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kuhakikisha wanalipa ushuru wa huduma vinginevyo Baraza hilo litachukua hatua za kisheria dhidi yao.


Kupitia kikao cha baraza la madiwani kilichoketi leo Agosti  23, 2024, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Mhe. Yanga Makaga amelazimika kuunda kamati ya wajumbe saba kwa ajili ya ufuatiliaji wa makampuni hayo ambayo yamekuwa yakikwepa kulipa ushuru wa huduma kwa Halmashauri kitendo kinachosababisha kutokufikia malengo ya Halamshauri kwenye ukusanyaji wa mapato.


"Waheshimiwa madiwani kwa hili hapana, tunatoa siku saba tofauti na hapo tutaitisha kikao kingine tufanye maamuzi juu ya wakandarasi hawa, na ninaunda kamati kufuatilia hili jambo" amesema Mhe. Makaga.


Diwani wa kata ya Tabaruka Mhe. Sospiter Busumabu amesema ni aibu kwa wakandarasi wanaofanya kazi kupitia wakala wa Barabara vijijini na Mjini (TARURA) kukwepa kulipa ushuru wa huduma na ameitaka TARURA iwajibike kwa kuwataka wakandarasi hao  kulipa ushuru wa huduma kwa Halmashauri kwani ni takwa la kisheria.


Diwani wa kata ya Kishinda Mhe. Vicent Shokolo amesema kitendo cha kutokukusanya ushuru wa huduma kutoka wakandarasi wanaofanya kazi na na baadhi ya taasisi ikiwemo TARURA kinakera na wamemtaka Meneja wa TARURA Wilaya ya Sengerema kuhakikisha anatoa ushirikiano kwa Halmashauri kwani zote ni taasisi za Serikali.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Binuru Shekidele amesema taasisi zote zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ikiwemo TARURA, SEUWASA, TANESCO na Mgodi wa Nyanzaga zimeandikiwa barua ya kukumbushia kampuni na wafanyabiashara wanaofanya kazi na taasisi hizo kuhakikisha wanalipa  ushuru wa huduma kwa Halmashauri.


Mbunge wa Jimbo la Sengerema Mhe. Hamis Tabasamu ameitaka TARURA na taasisi zingine kuhakikisha zinaelekeza makampuni na wafanya biashara wanaoingia mikataba nao kuhakikisha wanalipa tozo zote za Halmashauri kwani wamekuwa wakisaini mikataba mingi na kampuni hizo, hivyo hawapaswi kukwepa kulipa ushuru wa huduma.


Kwa mujibu wa sheria ya fedha ya Serikali za Mitaa sura ya 290 na marekebisho yake ya mwaka 2019 kifungu cha 6 mfanyabiashara yeyote mwenye leseni, kampuni, wakandarasi wanaofanya kazi ndani ya Halmashauri husika wanatakiwa kulipa ushuru wa huduma kwa Halmashauri husika isiyopungua asilimia 0.3 ya mauzo ghafi.


Kupitia kikao hicho Baraza la madiwani limemchagua tena Mhe. Makoye Sengerema diwani kata ya Sima kuendelea kuwa Makamu mwenyekiti wa Halmashauri kwa kipindi cha mwaka 2024/2025 ambapo pia zimeundwa kamati mbalimbali za kudumu.

Matangazo ya Kawaida

  • TAARIFA YA FEDHA YA HESABU ZA MWISHO HALMASHAURI YA WILAYA SENGEREMA KWA MWAKA ULIOISHIA TAREHE 30 JUNI 2024 August 06, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI MBALIMBALI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA SENGEREMA July 29, 2025
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MAKUBALIANO YA NYONGEZA KATI YA SERIKALI NA KAMPUNI YA NYANZAGA MINING COMPANY LIMITED KWA AJILI YA UCHIMBAJI MKUBWA WA MADINI YA DHAHABU

    August 20, 2025
  • MAADHIMISHO YA KILELE CHA JUMA LA ELIMU YA WATU WAZIMA HALMASHAURI YA WILAYA YA SENGEREMA

    August 20, 2025
  • MAFUNZO KWA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA HALMASHAURI YA WILAYA YA SENGEREMA

    August 04, 2025
  • MAADHIMISHO YA SIKU YA KUMBUKIZI YA MAUAJI YA WATU WENYE UALBINO

    July 29, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.