• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

BARAZA LA MADIWANI SENGEREMA LAPITISHA BAJETI YA BILIONI 56

Posted on: January 10th, 2023

Baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema tarehe 10 Januari, 2023 limepitisha mapendekezo ya mpango na bajeti ya mwaka 2023/2024 yenye kiasi cha shilingi 56,136,022,839.00 (Bilioni hamsini na sita, milioni miamoja thelathini na sita, elfu ishirini na mbili na mia nane thelathini na tisa bila senti) huku likisisitiza kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato.


Katika kikao hicho Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Yanga Makaga ameiagiza timu ya Menejimenti ya Halmashauri kuhakikisha inaweka mikakati madhubuti ya ukasanyaji wa mapato kwani bajeti pendekezwa kwa upande wa mapato ya ndani imeongezeka kwa asilimia 18 kutoka shilingi 2,749,992,000 ya mwaka 2022/2023 na kufikia shilingi 3,377,319,839.00.


"ongezeko la asilimia 18.5 la mapato ya ndani sio kidogo, Menejimenti fungeni mikanda, hatutarajii kushuka hapo, kila idara ihakikishe inakusanya mapato kwa asilimia 100" alisisitiza Mhe. Makaga huku akiwaomba madiwani hao kushirikiana na timu ya menejementi ili kufikia lengo la mapato.


Mbali na kupongeza bajeti hiyo, Baraza la Madiwani pia limeagiza menejimenti ya Halmashauri kuhakikisha wanawachukulia hatua kali wote wanaokwepa kulipa ushuru na tozo mbalimbali za Halmashauri.


Diwani wa kata ya Nyampande Mhe. George Kazungu amewaomba viongozi kuwa mfano bora kwenye ulipaji wa mapato ya Halmashauri ili iweze kufikia malengo ya kuwahudumia wananchi na amesisitiza uwepo wa takwimu sahihi za wafanayabiashara wanaotakiwa kulipa leseni za biashara katika mwaka husika.


Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Sengerema ndugu Jamary Athuman amelipongeza baraza hilo na timu ya menejimeti kwa ushirikiano mzuri uliopo baina ya Serikalia na CCM ambapo kumeifanya Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ipige hatua hivyo amelitaka baraza hilo kwenda kwa wananchi kiwaelezea mambo mazuri yanayotekelezwa na Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ndugu Binuru Shekidele amelishukuru baraza hilo kwa kukubali kupitisha mapendekezo hayo ya bajeti na ameahidi kuyafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa na baraza hilo.


Mapema akiwasilisha mapendekezo ya bajeti, afisa mipango wa Halmashauri ndugu Pastory Mukaruka amesema bajeti inayopendekezwa imeongezeka kwa asilimia 1.12 kutoka shilingi 55,505,703,000.00 ya mwaka 2022/2023 na kufikia shilingi 56,136,022,839.00. Katika bajeti hiyo Mishahara ni shilingi 38,583,256,000.00, Ruzuku ya matumizi mengineyo ni shilingi 1,115,111,000.00, Ruzuku ya miradi ya maendeleo shilingi 7,025,121,000.00 na Ruzuku ya Wafadhili ya miradi ya maendeleo ni shilingi 6,032,206,000.00

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.