• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

BARAZA LA MADIWANI SENGEREMA LAPITISHA BAJETI YA BILIONI

Posted on: January 17th, 2025

Stendi ya Kisasa na Soko Jipya Kujengwa Mjini Sengerema

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema leo Januari 17, 2025, limepitisha mpango na bajeti   wa mwaka 2025/2026 yenye jumla ya shilingi 66,308,388,446 huku likiweka vipaumbele vya kuanzisha miradi ya kimkakati ikiwemo kituo cha mabasi na soko mjini Sengerema.


Akifungua kikao hicho, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Mhe. Yanga Makaga amesema kwa mwaka 2024/2025 Serikali imeweza kutoa fedha nyingi za miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kitendo ambacho kimesababisha kuanzishwa na kukamilika kwa miradi mingi katika sekta zote hivyo ametoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali wananchi wa Sengerema.


"Bajeti ya 2023/2024 Sengerema tulivuka lengo kwa asilimia 115, kwa bajeti tuliyonayo sasa, tupo zaidi ya asilimia 55 ya lengo la bajeti, tumpongeze sana Mhe. Rais, mbunge wetu pamoja na timu ya Menejimenti kwa jitihada za kutufikisha hapa" amesema Mhe. Makaga.


Akiwasilisha bajeti hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Mkuu wa idara ya Mipango, Wilbard Bandola amesema katika bajeti  inayopendekezwa, vipaumbele ni pamoja na uanzishwaji wa miradi ya kimkakati yenye lengo la kuongeza mapato ikiwemo ujenzi wa kituo cha kisasa cha Mabasi pamoja na Soko mjini Sengerema kwa gharama ya shilingi 5,076,790,995.


Baadhi ya Madiwani wamesema kukamilika kwa daraja la Magufuli kutaisaidia Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kukua kiuchumi, hivyo miundombinu bora kama kituo cha mabasi cha kisasa na soko zuri haviepukiki na lengo likiwa ni kuimarisha shughuli za kiuchumi kwa Halmashauri ya Sengerema.


Katika bajeti hiyo Halmashauri inatarajiwa kukusanya mapato ya ndani jumla ya shilingi 3,312,209,446 ambapo fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo ni shilingi 17,312,559,000, amesema katika bajeti hiyo inakadiriwa kuwa na ruzuku ya mishahara yenye jumla ya shilingi 44,218,387,000 pamoja na matumizi mengineyo ya shilingi 1,465,228,000.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.