• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

BARAZA LA MADIWANI SENGEREMA LAPITISHA AZIMIO LA KUMPONGEZA DKT. SAMIA

Posted on: November 15th, 2024

Lampongeza Mbunge Tabasamu kwa Jitihada Binafsi Kuleta Maendeleo


Idara ya Afya Yapata Watumishi wapya 104


Baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema limepitisha azimio la kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan kutokana na kutoa fedha nyingi za miradi ya maendeleo kwa Halmashauri hiyo.


Azimio hilo la pongezi limetolewa kwenye kikao cha Baraza la Madiwani cha robo ya kwanza kilichofanyika tarehe 15 Novemba, 2024 kwenye ukumbi wa mikutano wa Bomani.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Mhe. Yanga Makaga amesema katika kipindi cha hivi karibuni Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema imekuwa ikipokea fedha nyingi za miradi ya maendeleo kupitia sekta zote hivyo ni vyema Baraza hilo likamshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa jitihada hizo za kuwaletea maendeleo wananchi wa Sengerema na Tanzania kwa ujumla.


"Hivi karibuni tumepokea fedha nyingi kupitia sekta ya Maji, Barabara, Afya na Elimu, bado haitoshi tumepokea watumishi zaidi ya mia moja wa idara ya afya, hii ni historia kubwa kwetu" amesema Mwenyekiti wa Halmashauri.


Mbunge wa jimbo la Sengerema Mhe. Hamis Tabasamu amesema Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema imepokea fedha nyingi za miradi ya Maendeleo ukilinganisha na kipindi kipindi kingine hivyo ni vyema Baraza hilo kwa kauli moja likampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa fedha nyingi za miradi ya maendeleo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema hususan ujenzi na ukarabati wa Barabara nyingi ambazo zilikuwa hazipitiki na sasa zinapitika, miradi ya  umeme, maji, afya na elimu.


Mhe. Tabasamu amesema kupitia fedha za mfuko wa jimbo, mapato ya ndani pamoja na fedha za wadau wengine zimefanikisha kujenga uwanja wa mpira wa miguu ulipo Mnadani mjini Sengerema hivyo ameomba ushirikiano huo ulipo baina ya viongozi wote uendelee ili Halmashauri iweze kufikia malengo yake kwa wakati.


Diwani wa kata ya Tabaruka Mhe. Sospter Busumabu amesema kutokana na fedha nyingi za miradi ya maendeleo ni vyema Baraza hilo likampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutokana na miradi mingi ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa katika katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri pasipo kuhusisha michango ya wananchi.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema, Binuru Shekidele amesema maendeleo yanayoonekana katika Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ni kutokana na ushirikiano ulipo baina ya viongozi ambapo amesema kutokana na ushirikiano huo umekuwa ukifanikisha mambo mbalimbali ikiwemo ukamilishaji wa miradi kwa wakati na kwa ufanisi mkubwa ambapo amemshukuru mbunge wa jimbo la Sengerema kwa utayari wake katika kushughulikia kero za wananchi wa Sengerema.


Wajumbe wa Baraza hilo pia wamepongeza Mhe. Tabasamu kwa jitihada za kuwaletea maendeleo wananchi wa Sengerema ambapo wamesema kwa jitihada zake binafsi amekuwa akifuatilia mambo mbalimbali na kufanikisha hivyo kuondoa changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi ikiwemo upatikanaji wa maji safi na salama, ubovu wa barabara, vituo vya afya na zahati, uanzishwaji wa shule mpya za msingi na sekondari pamoja na upatikanaji wa watumishi kwenye sekta ya afya na elimu.


Mwezi Oktoba Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema imepokea shilingi Bilioni 2.18 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo shilingi Bilioni 1.3 kwa ajili ya ukamilishaji wa jengo la Utawala la Halmashauri lililopo Bomani pamoja na sekta ya elimu na afya.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO AJIRA-UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA September 16, 2024
  • TANAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI SENGEREMA August 07, 2024
  • ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI UANDIKISHAJI NA BVR August 08, 2024
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • SENGEREMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MIKOPO YA MILIONI 362

    March 05, 2025
  • UMOJA WA WANAWAKE SENGEREMA WATOA MISAADA

    March 04, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • CHUO KIKUU CHA ARDHI 'KAMPASI' YA SENGEREMA KUANZA KUJENGWA FEBRUARI 2025

    February 03, 2025
  • Ona vyote

Video

DKT. SAMIA AKIWASALIMIA WANANCHI WA SENGEREMA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.