• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Sengerema District Council
Sengerema District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Usafishaji na Mazingira
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Tehama na Takwimu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • Mawasiliano Serikalini
      • Fedha na Uhasibu
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Maliasiri na Uhifadhi wa Mazingira
      • Taka ngumu na Usafishaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Majukumu ya Diwani katika Hamashauri
      • Wakuchaguliwa
      • Viti Maalumu
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Ukimwi
      • Elimu, Afya na Maji
      • Maadili
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingizira
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
    • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Majukumu ya Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Jarida Tando
    • Nyaraka
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

BARAZA LA MADIWANI SENGEREMA LAKOSHWA NA UKUSANYAJI WA MAPATO

Posted on: March 15th, 2023

Laipongeza Idara ya Elimu Sekondari kwa matokeo mazuri


Baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema limeipongeza timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kwa kusimamia vyema zoezi ukusanyaji wa mapato ya ndani pamoja na kusimamia vizuri upelekaji wa fedha za asilimia 40 za miradi ya maendeleo zitokanazo na mapato hayo.


Wakiongea kwa nyakati tofauti kwenye kikao cha Baraza hilo kilichofanyika leo jumatano tarehe 15 Machi, 2023, wajumbe hao wamesema kwa sasa ukusanyaji wa mapato unakwenda vizuri hivyo wameitaka timu ya Menejimenti kuhakikisha inabuni vyanzo vingine vya mapato ikiwemo uboreshaji wa stendi ya Mabasi ya Bukala na ile ya Mnadani pamoja na soko la Migombani ili kufikia lengo la ukusanyaji mapato ya ndani.


 Madiwani hao wamesema kitendo cha kusimamia vyema ukusanyaji wa mapato kunarahisisha shughuli mbalimbali za Halmashauri zikiwemo za ujenzi wa miradi inayotegemea mapato ya ndani na shughuli zingine za utoaji huduma kwa wananchi.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Mhe. Yanga Makaga amesema kwa sasa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema mambo mengi yanakwenda vizuri hivyo amewapongeza watumishi kwa kufanya kazi kwa kujituma na amewaomba madiwani kutoa ushirikiano ili kuweza kufikia malengo ikiwemo ukusanyaji wa mapato ya ndani.


"Halmashauri yetu kwa sasa imetulia, shughuli zinafanyika vizuri, ni vyema tuwe na tabia pia ya kuwapongeza watumishi wanapofanya vizuri" ameongeza kusema Mhe. Makaga.


Diwani wa kata ya Kahumulo ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira mhe. Fortunatus Nzwagi amesema kuna haja ya kuipongeza Menejimenti kwa ukusanyaji wa mapato ya ndani kwani kwa kufanya hivyo kumesababisha upelekaji wa fedha za miradi inayotokana na mapato ya ndani kufika kwa wakati.


Naye diwani wa kata ya Tabaruka mhe. Sospiter Busumabu amesema Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kwa sasa mambo mengi yanakwenda vizuri hivyo ameliomba Baraza hilo kumpongeza Mwenyekiti wa Halmashauri kwa usimamizi mzuri wa Halmashauri ikiwemo ukusanyaji wa mapato ya ndani na usimamizi miradi mbalimbali ya Halmashauri.


Hata hivyo diwani wa kata ya Igulumuki ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya Elimu mhe. Deus Ndaki ameipongeza Idara ya Elimu Sekondari kwa kusimamia vizuri taaluma kitendo kilichopelekea kuongezeka kwa ufaulu kwenye mtihani wa kidato cha nne 2022 na kupunguza daraja sifuri kwenye baadhi ya shule.


Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kwa mwaka wa fedha 2022/2023 imepanga kukusanya shilingi  2,043,228,000 za mapato ya ndani, ambapo hadi sasa kufikia mwezi Februari 2023 imekusanya shilingi 1,204,751,966.19  sawa na asilimia 58.96 ya lengo la mwaka, ambapo shilingi  476,522,413.99 tayari zimetolewa kwenda kwenye miradi ya maendeleo sawa na asilimia 60.17  ya lengo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI March 14, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI KADA YA DEREVA II NA MTUNZA KUMBUKUMBU II November 11, 2022
  • Majina ya walioitwa kwenye Mafunzo ya Ukarani, Tehama na Usimamizi wa Maudhui katika Sensa ya Mwaka 2022 July 26, 2022
  • Tangazo la kuitwa kwenye Usaili wa Kazi ya Afisa Mtendaji wa Kijiji Daraja III, Katibu Muhtasi Daraja III na Dereva Daraja II July 05, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI SENGEREMA LAKOSHWA NA UKUSANYAJI WA MAPATO

    March 15, 2023
  • DC SENGEREMA AKEMEA MMOMONYOKO WA MAADILI

    March 08, 2023
  • RC MALIMA ATIMIZA AHADI YAKE KWA WANANCHI WA MAMI

    March 08, 2023
  • BUYAGU KUWA KITUO CHA MFANO KILIMO CHA PAMBA

    March 02, 2023
  • Ona vyote

Video

RC ATOA SIKU NNE WAZAZI KUPELEKA WATOTO KIDATO CHA KWANZA
Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani Yetu
  • Jarida Tando la Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Utumishi wa Umma
  • OR-Tamisemi
  • OR-Ikulu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani Yetu

Mawasiliano

    Sengerema District Council

    Anuani ya Posta: Box 175

    Simu ya Mezani: 028 2590162

    Simu: 0688223308

    Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani Yetu

Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.