Kamati ya Mradi wa kuimarisha na kuboresha Elimu ya Awali na Msingi (BOOST) ya Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Jumatatu tarehe 21 Agosti, 2023 imetembelea na kukagua miradi katika shule zilizopokea fedha mwezi Mei 2023.
Mkuu wa Idara ya Elimu Msingi ndugu Donati Bunonos amesema katika shule zote zilizopokea fedha baadhi zimekamilisha na chache zilizobaki ziko katika hatua za ukamilishaji.
"Kwenye mradi huu tunaenda vizuri ni shule chache zinamalizia ujenzi na zimefikia asilimia 91 ni matarajio yetu ndani ya mwezi huu wa Agosti tutakuwa tumekamilisha katika shule zote" alisema ndugu Bunonos.
Mwezi Mei 2023, Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ilipokea fedha kiasi cha Tsh. Bilioni 1.6 kutoka Serikali kuu kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali katika jumla ya shule 11 ambapo shule mbili za Kilabela na Bungumbikiso zimejengewa shule mpya.
Sengerema District Council
Anuani ya Posta: Box 175
Simu ya Mezani: 028 2590162
Simu: 0688223308
Barua pepe: ded@sengeremadc.go.tz
Copyright ©2021 SENGEREMA DISTRICT COUNCIL . All rights reserved.